< Zaburi 132 >

1 Wimbo wa kwenda juu. Ee Bwana, mkumbuke Daudi na taabu zote alizozistahimili.
Canción de las gradas. Acuérdate, oh SEÑOR, de David, de toda su aflicción;
2 Aliapa kiapo kwa Bwana na akaweka nadhiri kwa Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo:
de cómo juró al SEÑOR, prometió al Fuerte de Jacob:
3 “Sitaingia nyumbani mwangu au kwenda kitandani mwangu:
No entraré en la morada de mi casa, ni subiré sobre el lecho de mi estrado;
4 sitaruhusu usingizi katika macho yangu, wala kope zangu kusinzia,
no daré sueño a mis ojos, ni a mis párpados adormecimiento,
5 mpaka nitakapompatia Bwana mahali, makao kwa ajili ya Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo.”
hasta que halle lugar para el SEÑOR, moradas para el Fuerte de Jacob.
6 Tulisikia habari hii huko Efrathi, tulikutana nayo katika mashamba ya Yaara:
He aquí, en Efrata oímos de ella; la hallamos en los campos del bosque.
7 “Twendeni kwenye makao yake, na tuabudu kwenye kiti cha kuwekea miguu yake;
Entraremos en sus tiendas; adoremos al estrado de sus pies.
8 inuka, Ee Bwana, uje mahali pako pa kupumzikia, wewe na Sanduku la nguvu zako.
Levántate, oh SEÑOR, a tu reposo; tú y el arca de tu fortaleza.
9 Makuhani wako na wavikwe haki, watakatifu wako na waimbe kwa furaha.”
Tus sacerdotes se vistan de justicia, y se regocijen tus misericordiosos.
10 Kwa ajili ya Daudi mtumishi wako, usimkatae mpakwa mafuta wako.
Por amor de David tu siervo no vuelvas de tu ungido el rostro.
11 Bwana alimwapia Daudi kiapo, kiapo cha uhakika ambacho hatakitangua: “Nitamweka mmoja wa wazao wako mwenyewe katika kiti chako cha enzi,
Juró el SEÑOR verdad a David, no se apartará de ella; del fruto de tu vientre pondré sobre tu trono.
12 kama wanao watashika Agano langu na sheria ninazowafundisha, ndipo wana wao watarithi kiti chako cha enzi milele na milele.”
Si tus hijos guardaren mi alianza, y mi testimonio que yo les enseñaré; sus hijos también se sentarán sobre tu trono para siempre.
13 Kwa maana Bwana ameichagua Sayuni, amepaonea shauku pawe maskani yake:
Porque el SEÑOR ha elegido a Sion; la deseó por habitación para sí.
14 “Hapa ni mahali pangu pa kupumzika milele na milele; hapa ndipo nitakapoketi nikitawala, kwa sababu nimepaonea shauku:
Este será mi reposo para siempre; aquí habitaré, porque la he deseado.
15 Nitambariki kwa kumpa mahitaji tele: nitashibisha maskini wake kwa chakula.
Bendeciré abundantemente su provisión; a sus pobres saciaré de pan.
16 Nitawavika makuhani wake wokovu, nao watakatifu wake watadumu wakiimba kwa furaha.
Y a sus sacerdotes vestiré de salud, y sus misericordiosos exultarán de gozo.
17 “Hapa nitamchipushia Daudi pembe, na kuweka taa kwa ajili ya masiya wangu.
Allí haré reverdecer el cuerno de David; yo he aparejado lámpara a mi ungido.
18 Adui zake nitawavika aibu, bali taji kichwani pake itangʼaa sana.”
A sus enemigos vestiré de confusión; y sobre él florecerá su corona.

< Zaburi 132 >