< Zaburi 132 >
1 Wimbo wa kwenda juu. Ee Bwana, mkumbuke Daudi na taabu zote alizozistahimili.
Cântico dos degraus: Lembra-te, SENHOR, de Davi, [e] de todas as aflições dele.
2 Aliapa kiapo kwa Bwana na akaweka nadhiri kwa Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo:
Ele, que jurou ao SENHOR, [e] fez um voto ao Poderoso de Jacó,
3 “Sitaingia nyumbani mwangu au kwenda kitandani mwangu:
[dizendo]: Não entrarei na tenda de minha casa, nem subirei no leito de minha cama;
4 sitaruhusu usingizi katika macho yangu, wala kope zangu kusinzia,
Não darei sono aos meus olhos, [nem] cochilo às minhas pálpebras;
5 mpaka nitakapompatia Bwana mahali, makao kwa ajili ya Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo.”
Enquanto eu não achar um lugar para o SENHOR, moradas para o Poderoso de Jacó.
6 Tulisikia habari hii huko Efrathi, tulikutana nayo katika mashamba ya Yaara:
Eis que ouvimos dela em Efrata, e [a] achamos nos campos de Jaar.
7 “Twendeni kwenye makao yake, na tuabudu kwenye kiti cha kuwekea miguu yake;
Entraremos em suas moradas, [e] nos prostraremos perante o escabelo de seus pés.
8 inuka, Ee Bwana, uje mahali pako pa kupumzikia, wewe na Sanduku la nguvu zako.
Levanta-te, SENHOR, a teu repouso; tu e a arca de teu poder.
9 Makuhani wako na wavikwe haki, watakatifu wako na waimbe kwa furaha.”
Que teus sacerdotes se vistam de justiça, e teus santos gritem de alegria.
10 Kwa ajili ya Daudi mtumishi wako, usimkatae mpakwa mafuta wako.
Por causa de Davi teu servo, não rejeites o rosto de teu ungido.
11 Bwana alimwapia Daudi kiapo, kiapo cha uhakika ambacho hatakitangua: “Nitamweka mmoja wa wazao wako mwenyewe katika kiti chako cha enzi,
O SENHOR jurou a Davi [com] fidelidade; dela não se desviará. [Ele disse]: Do fruto do teu ventre porei sobre o teu trono.
12 kama wanao watashika Agano langu na sheria ninazowafundisha, ndipo wana wao watarithi kiti chako cha enzi milele na milele.”
Se teus filhos guardarem meu pacto e meus testemunhos que eu lhes ensinar, também seus filhos se sentarão sobre teu trono para sempre.
13 Kwa maana Bwana ameichagua Sayuni, amepaonea shauku pawe maskani yake:
Porque o SENHOR escolheu a Sião, desejou-a para sua habitação,
14 “Hapa ni mahali pangu pa kupumzika milele na milele; hapa ndipo nitakapoketi nikitawala, kwa sababu nimepaonea shauku:
[Dizendo]: Este é o meu repouso para sempre; aqui habitarei, pois assim desejei.
15 Nitambariki kwa kumpa mahitaji tele: nitashibisha maskini wake kwa chakula.
Abençoarei seu sustento abundantemente, [e] fartarei seus necessitados de pão.
16 Nitawavika makuhani wake wokovu, nao watakatifu wake watadumu wakiimba kwa furaha.
E a seus sacerdotes vestirei de salvação; e seus santos gritarão de alegria abundantemente.
17 “Hapa nitamchipushia Daudi pembe, na kuweka taa kwa ajili ya masiya wangu.
Ali farei brotar o poder de Davi; e preparei uma lâmpada para o meu ungido.
18 Adui zake nitawavika aibu, bali taji kichwani pake itangʼaa sana.”
A seus inimigos vestirei de vergonha; mas sobre ele florescerá sua coroa.