< Zaburi 132 >

1 Wimbo wa kwenda juu. Ee Bwana, mkumbuke Daudi na taabu zote alizozistahimili.
Pieśń stopni. Na Dawida pomnij, Panie! na wszystkie utrapienia jego.
2 Aliapa kiapo kwa Bwana na akaweka nadhiri kwa Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo:
Który przysiągł Panu, a ślub uczynił mocarzowi Jakóbowemu, mówiąc:
3 “Sitaingia nyumbani mwangu au kwenda kitandani mwangu:
Zaiste nie wnijdę do przybytku domu mego, i nie wstąpię na posłanie łoża mego;
4 sitaruhusu usingizi katika macho yangu, wala kope zangu kusinzia,
I nie pozwolę snu oczom moim, ani powiekom moim drzemania,
5 mpaka nitakapompatia Bwana mahali, makao kwa ajili ya Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo.”
Dokąd nie znajdę miejsca dla Pana, na mieszkania mocarzowi Jakóbowemu.
6 Tulisikia habari hii huko Efrathi, tulikutana nayo katika mashamba ya Yaara:
Oto usłyszawszy o niej w Efracie, znaleźliśmy ją na polach leśnych.
7 “Twendeni kwenye makao yake, na tuabudu kwenye kiti cha kuwekea miguu yake;
Wnijdźmyż do przybytków jego, a kłaniajmy się u podnóżka nóg jego.
8 inuka, Ee Bwana, uje mahali pako pa kupumzikia, wewe na Sanduku la nguvu zako.
Powstańże Panie! a wnijdź do odpocznienia twego, ty, i skrzynia możności twojej.
9 Makuhani wako na wavikwe haki, watakatifu wako na waimbe kwa furaha.”
Kapłani twoi niech się obloką w sprawiedliwość, a święci twoi nie się rozradują.
10 Kwa ajili ya Daudi mtumishi wako, usimkatae mpakwa mafuta wako.
Dla Dawida, sługi twego, nie odwracaj oblicza pomazańca twego.
11 Bwana alimwapia Daudi kiapo, kiapo cha uhakika ambacho hatakitangua: “Nitamweka mmoja wa wazao wako mwenyewe katika kiti chako cha enzi,
Przysiągł Pan Dawidowi prawdę, a nie uchyli się od niej, mówiąc: Z owocu żywota twego posadzę na stolicy twojej.
12 kama wanao watashika Agano langu na sheria ninazowafundisha, ndipo wana wao watarithi kiti chako cha enzi milele na milele.”
Będąli strzegli synowie twoi przymierza mojego, i świadectw moich, których ich nauczę: tedy i synowie ich aż na wieki będą siedzieli na stolicy twojej
13 Kwa maana Bwana ameichagua Sayuni, amepaonea shauku pawe maskani yake:
Albowiem obrał Pan Syon, i upodobał go sobie na mieszkanie, mówiąc:
14 “Hapa ni mahali pangu pa kupumzika milele na milele; hapa ndipo nitakapoketi nikitawala, kwa sababu nimepaonea shauku:
Toć będzie odpocznienie moje aż na wieki; tu będę mieszkał, bom go siebie upodobał.
15 Nitambariki kwa kumpa mahitaji tele: nitashibisha maskini wake kwa chakula.
Żywność jego będę obficie błogosławił, a ubogich jego nasycę chlebem.
16 Nitawavika makuhani wake wokovu, nao watakatifu wake watadumu wakiimba kwa furaha.
Kapłanów jego przyoblokę zbawieniem, a święci jego weseląc się, radować się będą.
17 “Hapa nitamchipushia Daudi pembe, na kuweka taa kwa ajili ya masiya wangu.
Tam sprawię, że zakwitnie róg Dawidowy; tam zgotuję pochodnię pomazańcowi memu.
18 Adui zake nitawavika aibu, bali taji kichwani pake itangʼaa sana.”
Nieprzyjaciół jego przyoblokę wstydem; ale nad nim rozkwitnie się korona jego.

< Zaburi 132 >