< Zaburi 132 >
1 Wimbo wa kwenda juu. Ee Bwana, mkumbuke Daudi na taabu zote alizozistahimili.
En sang ved festreisene. Herre, gi David lønn for hans møie,
2 Aliapa kiapo kwa Bwana na akaweka nadhiri kwa Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo:
han som tilsvor Herren, gav Jakobs Veldige det løfte:
3 “Sitaingia nyumbani mwangu au kwenda kitandani mwangu:
Jeg vil ikke gå inn i mitt huses telt, jeg vil ikke stige op på min sengs leie,
4 sitaruhusu usingizi katika macho yangu, wala kope zangu kusinzia,
jeg vil ikke unne mine øine søvn, mine øielokk slummer,
5 mpaka nitakapompatia Bwana mahali, makao kwa ajili ya Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo.”
før jeg finner et sted for Herren, en bolig for Jakobs Veldige!
6 Tulisikia habari hii huko Efrathi, tulikutana nayo katika mashamba ya Yaara:
Se, vi hørte om den i Efrata, vi fant den i skogsbygden.
7 “Twendeni kwenye makao yake, na tuabudu kwenye kiti cha kuwekea miguu yake;
Vi vil komme til hans bolig, vi vil tilbede for hans føtters skammel.
8 inuka, Ee Bwana, uje mahali pako pa kupumzikia, wewe na Sanduku la nguvu zako.
Reis dig, Herre, og kom til ditt hvilested, du og din styrkes ark!
9 Makuhani wako na wavikwe haki, watakatifu wako na waimbe kwa furaha.”
La dine prester klæ sig i rettferd og dine fromme rope med fryd!
10 Kwa ajili ya Daudi mtumishi wako, usimkatae mpakwa mafuta wako.
For Davids, din tjeners skyld vise du ikke din salvedes åsyn tilbake!
11 Bwana alimwapia Daudi kiapo, kiapo cha uhakika ambacho hatakitangua: “Nitamweka mmoja wa wazao wako mwenyewe katika kiti chako cha enzi,
Herren har svoret David en sann ed, som han ikke vil gå fra: Av ditt livs frukt vil jeg sette konger på din trone;
12 kama wanao watashika Agano langu na sheria ninazowafundisha, ndipo wana wao watarithi kiti chako cha enzi milele na milele.”
dersom dine barn holder min pakt og mine vidnesbyrd, som jeg vil lære dem, da skal også deres barn for all tid sitte på dine trone.
13 Kwa maana Bwana ameichagua Sayuni, amepaonea shauku pawe maskani yake:
For Herren har utkåret Sion, han har attrådd det til sin bolig:
14 “Hapa ni mahali pangu pa kupumzika milele na milele; hapa ndipo nitakapoketi nikitawala, kwa sababu nimepaonea shauku:
Dette er mitt hvilested til evig tid; her vil jeg bo, fordi jeg har attrådd det.
15 Nitambariki kwa kumpa mahitaji tele: nitashibisha maskini wake kwa chakula.
Dets mat vil jeg velsigne, dets fattige vil jeg mette med brød,
16 Nitawavika makuhani wake wokovu, nao watakatifu wake watadumu wakiimba kwa furaha.
og dets prester vil jeg klæ med fryd.
17 “Hapa nitamchipushia Daudi pembe, na kuweka taa kwa ajili ya masiya wangu.
Der vil jeg la et horn vokse op for David, gjøre i stand en lampe for min salvede.
18 Adui zake nitawavika aibu, bali taji kichwani pake itangʼaa sana.”
Hans fiender vil jeg klæ i skam, men på ham skal hans krone stråle.