< Zaburi 132 >

1 Wimbo wa kwenda juu. Ee Bwana, mkumbuke Daudi na taabu zote alizozistahimili.
Ein Wallfahrtslied. Gedenke, HERR, dem David alle seine Mühsal,
2 Aliapa kiapo kwa Bwana na akaweka nadhiri kwa Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo:
ihm, der dem HERRN einst zuschwor
3 “Sitaingia nyumbani mwangu au kwenda kitandani mwangu:
»Wahrlich, ich will mein Wohnzelt nicht betreten, nicht mein Ruhelager besteigen;
4 sitaruhusu usingizi katika macho yangu, wala kope zangu kusinzia,
ich will meinen Augen den Schlaf nicht gönnen, nicht Schlummer meinen Augenlidern,
5 mpaka nitakapompatia Bwana mahali, makao kwa ajili ya Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo.”
bis eine Stätte dem HERRN ich gefunden, eine Wohnung für Jakobs mächtigen Gott!«
6 Tulisikia habari hii huko Efrathi, tulikutana nayo katika mashamba ya Yaara:
Ja, wir haben von ihr gehört in Ephrath, sie gefunden im Gefilde von Jaar:
7 “Twendeni kwenye makao yake, na tuabudu kwenye kiti cha kuwekea miguu yake;
»Laßt uns in seine Wohnung treten, uns niederwerfen vor dem Schemel seiner Füße!
8 inuka, Ee Bwana, uje mahali pako pa kupumzikia, wewe na Sanduku la nguvu zako.
Brich auf, o HERR, zu deiner Ruhstatt, du und die Lade (das Sinnbild) deiner Macht!
9 Makuhani wako na wavikwe haki, watakatifu wako na waimbe kwa furaha.”
Laß deine Priester sich kleiden in Gerechtigkeit, und deine Frommen mögen jubeln!
10 Kwa ajili ya Daudi mtumishi wako, usimkatae mpakwa mafuta wako.
Um deines Knechtes David willen weise das Antlitz deines Gesalbten nicht ab!«
11 Bwana alimwapia Daudi kiapo, kiapo cha uhakika ambacho hatakitangua: “Nitamweka mmoja wa wazao wako mwenyewe katika kiti chako cha enzi,
Geschworen hat der HERR dem David einen Eid, einen wahren Eid, von dem er nicht abgeht: »Von deinen leiblichen Sprossen will einen ich setzen auf deinen Thron.
12 kama wanao watashika Agano langu na sheria ninazowafundisha, ndipo wana wao watarithi kiti chako cha enzi milele na milele.”
Wenn deine Söhne meinen Bund beachten und meine Zeugnisse, die ich sie lehren werde, so sollen auch ihre Söhne für und für sitzen auf deinem Thron.«
13 Kwa maana Bwana ameichagua Sayuni, amepaonea shauku pawe maskani yake:
Denn der HERR hat Zion erwählt, hat es zu seiner Wohnung begehrt:
14 “Hapa ni mahali pangu pa kupumzika milele na milele; hapa ndipo nitakapoketi nikitawala, kwa sababu nimepaonea shauku:
»Dies ist meine Ruhstatt für immer, hier will ich wohnen, weil ich’s so begehrt.
15 Nitambariki kwa kumpa mahitaji tele: nitashibisha maskini wake kwa chakula.
Zions Nahrung will ich reichlich segnen, seine Armen sättigen mit Brot;
16 Nitawavika makuhani wake wokovu, nao watakatifu wake watadumu wakiimba kwa furaha.
seine Priester werde in Heil ich kleiden, seine Frommen sollen laut frohlocken.
17 “Hapa nitamchipushia Daudi pembe, na kuweka taa kwa ajili ya masiya wangu.
Dort will ich Davids Macht erblühen lassen; eine Leuchte hab’ ich meinem Gesalbten bereitet.
18 Adui zake nitawavika aibu, bali taji kichwani pake itangʼaa sana.”
Seine Feinde will ich kleiden in Schmach, doch ihm soll auf dem Haupt die Krone glänzen.«

< Zaburi 132 >