< Zaburi 132 >
1 Wimbo wa kwenda juu. Ee Bwana, mkumbuke Daudi na taabu zote alizozistahimili.
Ein Stufenlied. - Sei, Herr, zugunsten Davids eingedenk all dessen, was er gesprochen,
2 Aliapa kiapo kwa Bwana na akaweka nadhiri kwa Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo:
wie er dem Herrn geschworen, dem Starken Jakobs hat gelobt:
3 “Sitaingia nyumbani mwangu au kwenda kitandani mwangu:
"Ich gehe nimmer in mein Wohngezelt, besteige nicht mein Ruhebett,
4 sitaruhusu usingizi katika macho yangu, wala kope zangu kusinzia,
Versage meinen Augen Schlaf und Schlummer meinen Augenwimpern,
5 mpaka nitakapompatia Bwana mahali, makao kwa ajili ya Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo.”
bis daß ich eine Stätte finde für den Herrn, für Jakobs Starken eine Wohnung." -
6 Tulisikia habari hii huko Efrathi, tulikutana nayo katika mashamba ya Yaara:
Nun hörten wir davon zu Ephrat und fanden sie im Waldgefilde.
7 “Twendeni kwenye makao yake, na tuabudu kwenye kiti cha kuwekea miguu yake;
"Zu seiner Wohnung laßt uns gehen, vor seiner Füße Schemel niederfallen!"
8 inuka, Ee Bwana, uje mahali pako pa kupumzikia, wewe na Sanduku la nguvu zako.
Auf, Herr, zu Deiner Ruhestätte, Du und die Lade Deiner Herrscherwürde!
9 Makuhani wako na wavikwe haki, watakatifu wako na waimbe kwa furaha.”
Mit Heil laß Deine Priester sich bekleiden, und Deine Frommen mögen jubeln! -
10 Kwa ajili ya Daudi mtumishi wako, usimkatae mpakwa mafuta wako.
Um David, Deines Dieners willen, weis nicht zurück, den Du gesalbt!"
11 Bwana alimwapia Daudi kiapo, kiapo cha uhakika ambacho hatakitangua: “Nitamweka mmoja wa wazao wako mwenyewe katika kiti chako cha enzi,
Der Herr schwur David Dauer zu. Er geht davon nicht ab. "Auf deinen Thron erheb ich einen von deiner Leibesfrucht.
12 kama wanao watashika Agano langu na sheria ninazowafundisha, ndipo wana wao watarithi kiti chako cha enzi milele na milele.”
Bewahren deine Söhne meinen Bund und meine Zeugnisse, wie ich sie lehre, dann dürfen ihre Söhne allezeit auf deinem Throne sitzen!" -
13 Kwa maana Bwana ameichagua Sayuni, amepaonea shauku pawe maskani yake:
Der Herr hat Sion sich erkoren, zum Wohnsitz sich ersehen:
14 “Hapa ni mahali pangu pa kupumzika milele na milele; hapa ndipo nitakapoketi nikitawala, kwa sababu nimepaonea shauku:
"Das sei in Ewigkeit mein Ruhesitz, ich throne hier; denn hier gefällt es mir.
15 Nitambariki kwa kumpa mahitaji tele: nitashibisha maskini wake kwa chakula.
Ich segne seine Jugend und gebe seinen Armen Brot in Fülle.
16 Nitawavika makuhani wake wokovu, nao watakatifu wake watadumu wakiimba kwa furaha.
Mit Heil bekleid ich seine Priester, und frohe Lust sei seiner Frommen Teil!
17 “Hapa nitamchipushia Daudi pembe, na kuweka taa kwa ajili ya masiya wangu.
Ich lasse Davids Macht ersprossen, dem richt ich eine Leuchte her, den ich gesalbt.
18 Adui zake nitawavika aibu, bali taji kichwani pake itangʼaa sana.”
In Schande hüll ich seine Feinde, dieweil auf ihm ein Diadem erglänzt."