< Zaburi 132 >

1 Wimbo wa kwenda juu. Ee Bwana, mkumbuke Daudi na taabu zote alizozistahimili.
Cantique des degrés.
2 Aliapa kiapo kwa Bwana na akaweka nadhiri kwa Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo:
Comme il a juré au Seigneur, et voué ce vœu au Dieu de Jacob:
3 “Sitaingia nyumbani mwangu au kwenda kitandani mwangu:
Si j’entre dans l’intérieur de ma maison, si je monte sur le lit de mon repos;
4 sitaruhusu usingizi katika macho yangu, wala kope zangu kusinzia,
Si j’accorde à mes yeux le sommeil, et à mes paupières l’assoupissement;
5 mpaka nitakapompatia Bwana mahali, makao kwa ajili ya Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo.”
Et le repos à mes tempes, jusqu’à ce que je trouve un lieu pour le Seigneur, un tabernacle pour le Dieu de Jacob.
6 Tulisikia habari hii huko Efrathi, tulikutana nayo katika mashamba ya Yaara:
Voilà que nous avons appris qu’il était à Ephrata, nous l’avons trouvé dans les champs de la forêt.
7 “Twendeni kwenye makao yake, na tuabudu kwenye kiti cha kuwekea miguu yake;
Nous entrerons dans son tabernacle, nous adorerons dans le lieu où se sont arrêtés ses pieds,
8 inuka, Ee Bwana, uje mahali pako pa kupumzikia, wewe na Sanduku la nguvu zako.
Levez-vous, Seigneur, et entrez dans votre repos, vous et l’arche de votre sanctification.
9 Makuhani wako na wavikwe haki, watakatifu wako na waimbe kwa furaha.”
Que vos prêtres soient revêtus de justice et que vos saints exultent.
10 Kwa ajili ya Daudi mtumishi wako, usimkatae mpakwa mafuta wako.
À cause de David votre serviteur, ne détournez pas la face de votre christ.
11 Bwana alimwapia Daudi kiapo, kiapo cha uhakika ambacho hatakitangua: “Nitamweka mmoja wa wazao wako mwenyewe katika kiti chako cha enzi,
Dieu a juré la vérité à David, et il ne l’éludera pas: Je mettrai un fils du fruit de tes entrailles sur ton trône.
12 kama wanao watashika Agano langu na sheria ninazowafundisha, ndipo wana wao watarithi kiti chako cha enzi milele na milele.”
Si tes fils gardent mon alliance et mes témoignages que je leur enseignerai,
13 Kwa maana Bwana ameichagua Sayuni, amepaonea shauku pawe maskani yake:
Puisque le Seigneur a choisi Sion, il l’a choisi pour son habitation.
14 “Hapa ni mahali pangu pa kupumzika milele na milele; hapa ndipo nitakapoketi nikitawala, kwa sababu nimepaonea shauku:
C’est là pour toujours le lieu de mon repos, j’y habiterai, puisque je l’ai choisie.
15 Nitambariki kwa kumpa mahitaji tele: nitashibisha maskini wake kwa chakula.
Bénissant, je bénirai sa veuve: ses pauvres, je les rassasierai de pain.
16 Nitawavika makuhani wake wokovu, nao watakatifu wake watadumu wakiimba kwa furaha.
Je revêtirai ses prêtres du salut, et ses saints exulteront d’exultation.
17 “Hapa nitamchipushia Daudi pembe, na kuweka taa kwa ajili ya masiya wangu.
Là je produirai la corne de David: j’ai préparé une lampe à mon christ.
18 Adui zake nitawavika aibu, bali taji kichwani pake itangʼaa sana.”
Je couvrirai ses ennemis de confusion, mais sur lui fleurira ma sanctification.

< Zaburi 132 >