< Zaburi 132 >
1 Wimbo wa kwenda juu. Ee Bwana, mkumbuke Daudi na taabu zote alizozistahimili.
Cantique des pèlerinages. Éternel, souviens-toi de David Et de ses pénibles labeurs,
2 Aliapa kiapo kwa Bwana na akaweka nadhiri kwa Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo:
Lui qui fit ce serment à l'Éternel Et ce voeu au Puissant de Jacob:
3 “Sitaingia nyumbani mwangu au kwenda kitandani mwangu:
«Je n'entrerai pas dans la tente où j'habite, Et je ne monterai pas sur le lit où je repose;
4 sitaruhusu usingizi katika macho yangu, wala kope zangu kusinzia,
Je ne donnerai pas de sommeil à mes yeux. Ni de repos à, mes paupières,
5 mpaka nitakapompatia Bwana mahali, makao kwa ajili ya Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo.”
Avant d'avoir trouvé une résidence pour l'Éternel, Une demeure pour le Puissant de Jacob!»
6 Tulisikia habari hii huko Efrathi, tulikutana nayo katika mashamba ya Yaara:
Nous avions entendu dire que l'arche était à Éphrath, Et nous l'avons trouvée dans les champs de Jaar.
7 “Twendeni kwenye makao yake, na tuabudu kwenye kiti cha kuwekea miguu yake;
Entrons dans la demeure de l'Éternel; Prosternons-nous devant son marchepied;
8 inuka, Ee Bwana, uje mahali pako pa kupumzikia, wewe na Sanduku la nguvu zako.
Lève-toi, ô Éternel, viens dans ton lieu de repos, Toi et l'arche où ta majesté réside!
9 Makuhani wako na wavikwe haki, watakatifu wako na waimbe kwa furaha.”
Que tes sacrificateurs se parent de leurs vêtements sacrés, Et que tes fidèles poussent des cris de joie!
10 Kwa ajili ya Daudi mtumishi wako, usimkatae mpakwa mafuta wako.
Pour l'amour de David, ton serviteur, Ne repousse pas la face de ton Oint!
11 Bwana alimwapia Daudi kiapo, kiapo cha uhakika ambacho hatakitangua: “Nitamweka mmoja wa wazao wako mwenyewe katika kiti chako cha enzi,
L'Éternel a fait à David ce serment immuable, Et il ne le révoquera point: «Je mettrai sur ton trône un fils issu de toi.
12 kama wanao watashika Agano langu na sheria ninazowafundisha, ndipo wana wao watarithi kiti chako cha enzi milele na milele.”
Si tes enfants gardent mon alliance Et les enseignements que je leur donnerai, Leurs fils aussi, à perpétuité, Seront assis sur ton trône.»
13 Kwa maana Bwana ameichagua Sayuni, amepaonea shauku pawe maskani yake:
L'Éternel a fait choix de Jérusalem: Il a désiré en faire son séjour.
14 “Hapa ni mahali pangu pa kupumzika milele na milele; hapa ndipo nitakapoketi nikitawala, kwa sababu nimepaonea shauku:
«Cette ville est le lieu de mon repos, à perpétuité; Elle est la résidence que j'ai désirée.
15 Nitambariki kwa kumpa mahitaji tele: nitashibisha maskini wake kwa chakula.
Je remplirai de provisions ses greniers; Je rassasierai de pain ses indigents.
16 Nitawavika makuhani wake wokovu, nao watakatifu wake watadumu wakiimba kwa furaha.
Je donnerai pour vêtements à ses sacrificateurs Le salut qui vient de moi, Et ses fidèles pousseront des cris d'allégresse.
17 “Hapa nitamchipushia Daudi pembe, na kuweka taa kwa ajili ya masiya wangu.
C'est là que je ferai croître la puissance de David; C'est là que j'ai préparé un flambeau pour mon Oint.
18 Adui zake nitawavika aibu, bali taji kichwani pake itangʼaa sana.”
Je couvrirai de honte ses ennemis. Et sur sa tête brillera son diadème!»