< Zaburi 132 >
1 Wimbo wa kwenda juu. Ee Bwana, mkumbuke Daudi na taabu zote alizozistahimili.
Cantique graduel. Éternel, souviens-toi de David, et de toutes ses tribulations!
2 Aliapa kiapo kwa Bwana na akaweka nadhiri kwa Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo:
Il fit à l'Éternel ce serment, ce vœu au Dieu puissant de Jacob:
3 “Sitaingia nyumbani mwangu au kwenda kitandani mwangu:
« Je ne rentre point sous le toit de ma maison, et je ne monte point vers le lit où je repose;
4 sitaruhusu usingizi katika macho yangu, wala kope zangu kusinzia,
je n'accorde ni le dormir à mes yeux, ni le sommeil à mes paupières,
5 mpaka nitakapompatia Bwana mahali, makao kwa ajili ya Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo.”
que je n'aie trouvé un séjour pour l'Éternel, une demeure pour le Dieu puissant de Jacob. »
6 Tulisikia habari hii huko Efrathi, tulikutana nayo katika mashamba ya Yaara:
Voici, nous apprenions qu'elle était à Ephrata, puis nous la trouvions dans les champs de Jahar.
7 “Twendeni kwenye makao yake, na tuabudu kwenye kiti cha kuwekea miguu yake;
Rendons-nous à Sa demeure, prosternons-nous devant Son marchepied!
8 inuka, Ee Bwana, uje mahali pako pa kupumzikia, wewe na Sanduku la nguvu zako.
Lève-toi, Éternel, viens à ton lieu de repos, toi, et l'arche de ta majesté!
9 Makuhani wako na wavikwe haki, watakatifu wako na waimbe kwa furaha.”
Que tes prêtres soient vêtus de la grâce, et que tes saints poussent des cris de joie!
10 Kwa ajili ya Daudi mtumishi wako, usimkatae mpakwa mafuta wako.
Pour l'amour de David, ton serviteur, ne rebute pas ton Oint!
11 Bwana alimwapia Daudi kiapo, kiapo cha uhakika ambacho hatakitangua: “Nitamweka mmoja wa wazao wako mwenyewe katika kiti chako cha enzi,
L'Éternel fit à David un serment véridique, Il n'en reviendra point: « Je mettrai sur ton trône un fruit de tes entrailles.
12 kama wanao watashika Agano langu na sheria ninazowafundisha, ndipo wana wao watarithi kiti chako cha enzi milele na milele.”
Si tes fils gardent mon alliance et les lois que je leur enseigne, leurs enfants aussi à jamais seront assis sur ton trône. »
13 Kwa maana Bwana ameichagua Sayuni, amepaonea shauku pawe maskani yake:
Oui, l'Éternel a fait choix de Sion, Il veut y fixer sa demeure.
14 “Hapa ni mahali pangu pa kupumzika milele na milele; hapa ndipo nitakapoketi nikitawala, kwa sababu nimepaonea shauku:
« C'est ici pour jamais le lieu de mon repos, je veux y demeurer, car je l'ai choisie.
15 Nitambariki kwa kumpa mahitaji tele: nitashibisha maskini wake kwa chakula.
Je veux bénir sa nourriture, et rassasier de pain ses indigents.
16 Nitawavika makuhani wake wokovu, nao watakatifu wake watadumu wakiimba kwa furaha.
Et je revêtirai ses prêtres de salut, et ses saints pousseront des cris de joie.
17 “Hapa nitamchipushia Daudi pembe, na kuweka taa kwa ajili ya masiya wangu.
Là j'élèverai la puissance de David, et je tiendrai devant mon Oint un flambeau.
18 Adui zake nitawavika aibu, bali taji kichwani pake itangʼaa sana.”
Je revêtirai ses ennemis d'opprobre, et sur sa tête son diadème brillera. »