< Zaburi 132 >
1 Wimbo wa kwenda juu. Ee Bwana, mkumbuke Daudi na taabu zote alizozistahimili.
Cantique des degrés. Éternel, souviens-toi de David, De toutes ses peines!
2 Aliapa kiapo kwa Bwana na akaweka nadhiri kwa Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo:
Il jura à l’Éternel, Il fit ce vœu au puissant de Jacob:
3 “Sitaingia nyumbani mwangu au kwenda kitandani mwangu:
Je n’entrerai pas dans la tente où j’habite, Je ne monterai pas sur le lit où je repose,
4 sitaruhusu usingizi katika macho yangu, wala kope zangu kusinzia,
Je ne donnerai ni sommeil à mes yeux, Ni assoupissement à mes paupières,
5 mpaka nitakapompatia Bwana mahali, makao kwa ajili ya Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo.”
Jusqu’à ce que j’aie trouvé un lieu pour l’Éternel, Une demeure pour le puissant de Jacob.
6 Tulisikia habari hii huko Efrathi, tulikutana nayo katika mashamba ya Yaara:
Voici, nous en entendîmes parler à Éphrata, Nous la trouvâmes dans les champs de Jaar…
7 “Twendeni kwenye makao yake, na tuabudu kwenye kiti cha kuwekea miguu yake;
Allons à sa demeure, Prosternons-nous devant son marchepied!…
8 inuka, Ee Bwana, uje mahali pako pa kupumzikia, wewe na Sanduku la nguvu zako.
Lève-toi, Éternel, viens à ton lieu de repos, Toi et l’arche de ta majesté!
9 Makuhani wako na wavikwe haki, watakatifu wako na waimbe kwa furaha.”
Que tes sacrificateurs soient revêtus de justice, Et que tes fidèles poussent des cris de joie!
10 Kwa ajili ya Daudi mtumishi wako, usimkatae mpakwa mafuta wako.
A cause de David, ton serviteur, Ne repousse pas ton oint!
11 Bwana alimwapia Daudi kiapo, kiapo cha uhakika ambacho hatakitangua: “Nitamweka mmoja wa wazao wako mwenyewe katika kiti chako cha enzi,
L’Éternel a juré la vérité à David, Il n’en reviendra pas; Je mettrai sur ton trône un fruit de tes entrailles.
12 kama wanao watashika Agano langu na sheria ninazowafundisha, ndipo wana wao watarithi kiti chako cha enzi milele na milele.”
Si tes fils observent mon alliance Et mes préceptes que je leur enseigne, Leurs fils aussi pour toujours Seront assis sur ton trône.
13 Kwa maana Bwana ameichagua Sayuni, amepaonea shauku pawe maskani yake:
Oui, l’Éternel a choisi Sion, Il l’a désirée pour sa demeure:
14 “Hapa ni mahali pangu pa kupumzika milele na milele; hapa ndipo nitakapoketi nikitawala, kwa sababu nimepaonea shauku:
C’est mon lieu de repos à toujours; J’y habiterai, car je l’ai désirée.
15 Nitambariki kwa kumpa mahitaji tele: nitashibisha maskini wake kwa chakula.
Je bénirai sa nourriture, Je rassasierai de pain ses indigents;
16 Nitawavika makuhani wake wokovu, nao watakatifu wake watadumu wakiimba kwa furaha.
Je revêtirai de salut ses sacrificateurs, Et ses fidèles pousseront des cris de joie.
17 “Hapa nitamchipushia Daudi pembe, na kuweka taa kwa ajili ya masiya wangu.
Là j’élèverai la puissance de David, Je préparerai une lampe à mon oint,
18 Adui zake nitawavika aibu, bali taji kichwani pake itangʼaa sana.”
Je revêtirai de honte ses ennemis, Et sur lui brillera sa couronne.