< Zaburi 132 >
1 Wimbo wa kwenda juu. Ee Bwana, mkumbuke Daudi na taabu zote alizozistahimili.
Cantique des degrés. Éternel, souviens-toi de David, [et] de toutes ses afflictions!
2 Aliapa kiapo kwa Bwana na akaweka nadhiri kwa Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo:
Comment il a juré à l’Éternel, [et] fait un vœu au Puissant de Jacob:
3 “Sitaingia nyumbani mwangu au kwenda kitandani mwangu:
Si j’entre dans la demeure de ma maison, si je monte sur le lit où je couche,
4 sitaruhusu usingizi katika macho yangu, wala kope zangu kusinzia,
Si je permets à mes yeux de dormir, à mes paupières de sommeiller,
5 mpaka nitakapompatia Bwana mahali, makao kwa ajili ya Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo.”
Jusqu’à ce que j’aie trouvé un lieu pour l’Éternel, des demeures pour le Puissant de Jacob!
6 Tulisikia habari hii huko Efrathi, tulikutana nayo katika mashamba ya Yaara:
Voici, nous avons entendu parler d’elle à Éphrata, nous l’avons trouvée dans les champs de Jaar.
7 “Twendeni kwenye makao yake, na tuabudu kwenye kiti cha kuwekea miguu yake;
Entrons dans ses demeures, prosternons-nous devant le marchepied de ses pieds.
8 inuka, Ee Bwana, uje mahali pako pa kupumzikia, wewe na Sanduku la nguvu zako.
Lève-toi, Éternel! pour [entrer dans] ton repos, toi et l’arche de ta force!
9 Makuhani wako na wavikwe haki, watakatifu wako na waimbe kwa furaha.”
Que tes sacrificateurs soient revêtus de justice, et que tes saints chantent de joie.
10 Kwa ajili ya Daudi mtumishi wako, usimkatae mpakwa mafuta wako.
À cause de David, ton serviteur, ne repousse pas la face de ton oint.
11 Bwana alimwapia Daudi kiapo, kiapo cha uhakika ambacho hatakitangua: “Nitamweka mmoja wa wazao wako mwenyewe katika kiti chako cha enzi,
L’Éternel a juré à David [en] vérité, il n’en reviendra pas: Je mettrai du fruit de ton ventre sur ton trône.
12 kama wanao watashika Agano langu na sheria ninazowafundisha, ndipo wana wao watarithi kiti chako cha enzi milele na milele.”
Si tes enfants gardent mon alliance et mes témoignages que je leur enseignerai, leurs fils aussi seront assis à perpétuité sur ton trône.
13 Kwa maana Bwana ameichagua Sayuni, amepaonea shauku pawe maskani yake:
Car l’Éternel a choisi Sion; il l’a désirée pour être son habitation:
14 “Hapa ni mahali pangu pa kupumzika milele na milele; hapa ndipo nitakapoketi nikitawala, kwa sababu nimepaonea shauku:
C’est ici mon repos à perpétuité; ici j’habiterai, car je l’ai désirée.
15 Nitambariki kwa kumpa mahitaji tele: nitashibisha maskini wake kwa chakula.
Je bénirai abondamment ses vivres, je rassasierai de pain ses pauvres;
16 Nitawavika makuhani wake wokovu, nao watakatifu wake watadumu wakiimba kwa furaha.
Et je revêtirai de salut ses sacrificateurs, et ses saints exulteront en chantant de joie.
17 “Hapa nitamchipushia Daudi pembe, na kuweka taa kwa ajili ya masiya wangu.
Là je ferai germer la corne de David, j’ai préparé une lampe à mon oint.
18 Adui zake nitawavika aibu, bali taji kichwani pake itangʼaa sana.”
Je revêtirai de honte ses ennemis; et sur lui fleurira sa couronne.