< Zaburi 132 >

1 Wimbo wa kwenda juu. Ee Bwana, mkumbuke Daudi na taabu zote alizozistahimili.
Cantique des montées. Souviens-toi, Yahweh, de David, de toutes ses peines!
2 Aliapa kiapo kwa Bwana na akaweka nadhiri kwa Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo:
Il fit ce serment à Yahweh, ce vœu au Fort de Jacob:
3 “Sitaingia nyumbani mwangu au kwenda kitandani mwangu:
« Je n'entrerai pas dans la tente où j'habite, je ne monterai pas sur le lit où je repose;
4 sitaruhusu usingizi katika macho yangu, wala kope zangu kusinzia,
je n'accorderai point de sommeil à mes yeux, ni d'assoupissement à mes paupières,
5 mpaka nitakapompatia Bwana mahali, makao kwa ajili ya Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo.”
jusqu'à ce que j'aie trouvé un lieu pour Yahweh, une demeure pour le Fort de Jacob. »
6 Tulisikia habari hii huko Efrathi, tulikutana nayo katika mashamba ya Yaara:
Voici, entendions-nous dire, qu'elle est à Ephrata; nous l'avons trouvée dans les champs de Jaar.
7 “Twendeni kwenye makao yake, na tuabudu kwenye kiti cha kuwekea miguu yake;
Allons au tabernacle de Yahweh, prosternons-nous devant l'escabeau de ses pieds.
8 inuka, Ee Bwana, uje mahali pako pa kupumzikia, wewe na Sanduku la nguvu zako.
Lève-toi, Yahweh, viens au lieu de ton repos, toi et l'arche de ta majesté!
9 Makuhani wako na wavikwe haki, watakatifu wako na waimbe kwa furaha.”
Que tes prêtres soient revêtus de justice, et que tes fidèles poussent des cris d'allégresse!
10 Kwa ajili ya Daudi mtumishi wako, usimkatae mpakwa mafuta wako.
A cause de David, ton serviteur, ne repousse pas la face de ton Oint!
11 Bwana alimwapia Daudi kiapo, kiapo cha uhakika ambacho hatakitangua: “Nitamweka mmoja wa wazao wako mwenyewe katika kiti chako cha enzi,
Yahweh a juré à David la vérité, il ne s'en départira pas: « C'est du fruit de tes entrailles, que je mettrai sur ton trône.
12 kama wanao watashika Agano langu na sheria ninazowafundisha, ndipo wana wao watarithi kiti chako cha enzi milele na milele.”
Si tes fils gardent mon alliance, et les préceptes que je leur enseignerai, leurs fils aussi, à tout jamais, seront assis sur ton trône. »
13 Kwa maana Bwana ameichagua Sayuni, amepaonea shauku pawe maskani yake:
Car Yahweh a choisi Sion, il l'a désirée pour sa demeure.
14 “Hapa ni mahali pangu pa kupumzika milele na milele; hapa ndipo nitakapoketi nikitawala, kwa sababu nimepaonea shauku:
« C'est le lieu de mon repos pour toujours; j'y habiterai, car je l'ai désirée.
15 Nitambariki kwa kumpa mahitaji tele: nitashibisha maskini wake kwa chakula.
Je répandrai de riches bénédictions sur sa subsistance, je rassasierai de pain ses pauvres.
16 Nitawavika makuhani wake wokovu, nao watakatifu wake watadumu wakiimba kwa furaha.
Je revêtirai de salut ses prêtres, et ses fidèles pousseront des cris d'allégresse.
17 “Hapa nitamchipushia Daudi pembe, na kuweka taa kwa ajili ya masiya wangu.
Là je ferai grandir la puissance de David, je préparerai un flambeau à mon Oint.
18 Adui zake nitawavika aibu, bali taji kichwani pake itangʼaa sana.”
Je revêtirai de honte ses ennemis, et sur son front resplendira son diadème. »

< Zaburi 132 >