< Zaburi 132 >

1 Wimbo wa kwenda juu. Ee Bwana, mkumbuke Daudi na taabu zote alizozistahimili.
A song of ascents. Remember, O Lord, David all his sufferings,
2 Aliapa kiapo kwa Bwana na akaweka nadhiri kwa Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo:
the oath that he swore to the Lord, and his vow to the Strong One of Jacob,
3 “Sitaingia nyumbani mwangu au kwenda kitandani mwangu:
never to enter his tent, never to lie on his bed,
4 sitaruhusu usingizi katika macho yangu, wala kope zangu kusinzia,
never to give his eyes sleep or his eyelids slumber,
5 mpaka nitakapompatia Bwana mahali, makao kwa ajili ya Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo.”
till he had found a place for the Lord, for the Strong One of Jacob to live in.
6 Tulisikia habari hii huko Efrathi, tulikutana nayo katika mashamba ya Yaara:
We heard of it in Ephrathah, in the fields of Jaar we found it.
7 “Twendeni kwenye makao yake, na tuabudu kwenye kiti cha kuwekea miguu yake;
We went to the place where he dwelt, we bowed ourselves low at his footstool.
8 inuka, Ee Bwana, uje mahali pako pa kupumzikia, wewe na Sanduku la nguvu zako.
“Arise, Lord, and enter your resting-place, you and your mighty ark.
9 Makuhani wako na wavikwe haki, watakatifu wako na waimbe kwa furaha.”
Let your priests wear a garment of righteousness, your faithful shout aloud for joy.
10 Kwa ajili ya Daudi mtumishi wako, usimkatae mpakwa mafuta wako.
For the sake of David your servant, do not reject your Anointed.”
11 Bwana alimwapia Daudi kiapo, kiapo cha uhakika ambacho hatakitangua: “Nitamweka mmoja wa wazao wako mwenyewe katika kiti chako cha enzi,
The Lord swore an oath to David an oath that he will not break; “I will set on your throne a prince of your line.
12 kama wanao watashika Agano langu na sheria ninazowafundisha, ndipo wana wao watarithi kiti chako cha enzi milele na milele.”
If your sons keep my covenant and the statutes I teach them, then their sons, too, forever, will sit on your throne.”
13 Kwa maana Bwana ameichagua Sayuni, amepaonea shauku pawe maskani yake:
For the choice of the Lord is Zion; she is the home of his heart.
14 “Hapa ni mahali pangu pa kupumzika milele na milele; hapa ndipo nitakapoketi nikitawala, kwa sababu nimepaonea shauku:
“This is forever my resting-place, this is the home of my heart.
15 Nitambariki kwa kumpa mahitaji tele: nitashibisha maskini wake kwa chakula.
I will royally bless her provision, and give bread to her poor in abundance.
16 Nitawavika makuhani wake wokovu, nao watakatifu wake watadumu wakiimba kwa furaha.
Her priests I will clothe with salvation; her faithful will shout for joy.
17 “Hapa nitamchipushia Daudi pembe, na kuweka taa kwa ajili ya masiya wangu.
There will I raise up for David a dynasty of power. I have set my anointed a lamp that shall never go out.
18 Adui zake nitawavika aibu, bali taji kichwani pake itangʼaa sana.”
Robes of shame I will put on his foes, but on his head a glittering crown.”

< Zaburi 132 >