< Zaburi 132 >

1 Wimbo wa kwenda juu. Ee Bwana, mkumbuke Daudi na taabu zote alizozistahimili.
A SONG OF THE ASCENTS. Remember, YHWH, for David, all his afflictions;
2 Aliapa kiapo kwa Bwana na akaweka nadhiri kwa Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo:
Who has sworn to YHWH, He has vowed to the Mighty One of Jacob:
3 “Sitaingia nyumbani mwangu au kwenda kitandani mwangu:
“If I enter into the tent of my house, If I go up on the couch of my bed,
4 sitaruhusu usingizi katika macho yangu, wala kope zangu kusinzia,
If I give sleep to my eyes, To my eyelids—slumber,
5 mpaka nitakapompatia Bwana mahali, makao kwa ajili ya Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo.”
Until I find a place for YHWH, dwelling places for the Mighty One of Jacob.”
6 Tulisikia habari hii huko Efrathi, tulikutana nayo katika mashamba ya Yaara:
Behold, we have heard it in Ephratah, We have found it in the fields of the forest.
7 “Twendeni kwenye makao yake, na tuabudu kwenye kiti cha kuwekea miguu yake;
We come into His dwelling places, We bow ourselves at His footstool.
8 inuka, Ee Bwana, uje mahali pako pa kupumzikia, wewe na Sanduku la nguvu zako.
Arise, O YHWH, to Your rest, You, and the Ark of Your strength,
9 Makuhani wako na wavikwe haki, watakatifu wako na waimbe kwa furaha.”
Your priests put on righteousness, And Your pious ones cry aloud.
10 Kwa ajili ya Daudi mtumishi wako, usimkatae mpakwa mafuta wako.
For the sake of Your servant David, Do not turn back the face of Your anointed.
11 Bwana alimwapia Daudi kiapo, kiapo cha uhakika ambacho hatakitangua: “Nitamweka mmoja wa wazao wako mwenyewe katika kiti chako cha enzi,
YHWH has sworn truth to David, He does not turn back from it: “Of the fruit of your body, I set on the throne for you.
12 kama wanao watashika Agano langu na sheria ninazowafundisha, ndipo wana wao watarithi kiti chako cha enzi milele na milele.”
If your sons keep My covenant, And My testimonies that I teach them, Their sons also forever and ever Sit on the throne for you.”
13 Kwa maana Bwana ameichagua Sayuni, amepaonea shauku pawe maskani yake:
For YHWH has fixed on Zion, He has desired [it] for a seat to Himself,
14 “Hapa ni mahali pangu pa kupumzika milele na milele; hapa ndipo nitakapoketi nikitawala, kwa sababu nimepaonea shauku:
“This [is] My rest forever and ever, Here I sit, for I have desired it.
15 Nitambariki kwa kumpa mahitaji tele: nitashibisha maskini wake kwa chakula.
I greatly bless her provision, I satisfy her poor [with] bread,
16 Nitawavika makuhani wake wokovu, nao watakatifu wake watadumu wakiimba kwa furaha.
And I clothe her priests [with] salvation, And her pious ones sing aloud.
17 “Hapa nitamchipushia Daudi pembe, na kuweka taa kwa ajili ya masiya wangu.
There I cause a horn to spring up for David, I have arranged a lamp for My Anointed.
18 Adui zake nitawavika aibu, bali taji kichwani pake itangʼaa sana.”
I clothe His enemies [with] shame, And His crown flourishes on Him!”

< Zaburi 132 >