< Zaburi 132 >

1 Wimbo wa kwenda juu. Ee Bwana, mkumbuke Daudi na taabu zote alizozistahimili.
Lord, remember David, and all his afflictions:
2 Aliapa kiapo kwa Bwana na akaweka nadhiri kwa Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo:
How he swore to the LORD, and vowed to the mighty God of Jacob;
3 “Sitaingia nyumbani mwangu au kwenda kitandani mwangu:
Surely I will not come into the tabernacle of my house, nor go up into my bed;
4 sitaruhusu usingizi katika macho yangu, wala kope zangu kusinzia,
I will not give sleep to my eyes, or slumber to my eyelids,
5 mpaka nitakapompatia Bwana mahali, makao kwa ajili ya Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo.”
Until I find out a place for the LORD, an habitation for the mighty God of Jacob.
6 Tulisikia habari hii huko Efrathi, tulikutana nayo katika mashamba ya Yaara:
See, we heard of it at Ephratah: we found it in the fields of the wood.
7 “Twendeni kwenye makao yake, na tuabudu kwenye kiti cha kuwekea miguu yake;
We will go into his tabernacles: we will worship at his footstool.
8 inuka, Ee Bwana, uje mahali pako pa kupumzikia, wewe na Sanduku la nguvu zako.
Arise, O LORD, into your rest; you, and the ark of your strength.
9 Makuhani wako na wavikwe haki, watakatifu wako na waimbe kwa furaha.”
Let your priests be clothed with righteousness; and let your saints shout for joy.
10 Kwa ajili ya Daudi mtumishi wako, usimkatae mpakwa mafuta wako.
For your servant David’s sake turn not away the face of your anointed.
11 Bwana alimwapia Daudi kiapo, kiapo cha uhakika ambacho hatakitangua: “Nitamweka mmoja wa wazao wako mwenyewe katika kiti chako cha enzi,
The LORD has sworn in truth to David; he will not turn from it; Of the fruit of your body will I set on your throne.
12 kama wanao watashika Agano langu na sheria ninazowafundisha, ndipo wana wao watarithi kiti chako cha enzi milele na milele.”
If your children will keep my covenant and my testimony that I shall teach them, their children shall also sit on your throne for ever more.
13 Kwa maana Bwana ameichagua Sayuni, amepaonea shauku pawe maskani yake:
For the LORD has chosen Zion; he has desired it for his habitation.
14 “Hapa ni mahali pangu pa kupumzika milele na milele; hapa ndipo nitakapoketi nikitawala, kwa sababu nimepaonea shauku:
This is my rest for ever: here will I dwell; for I have desired it.
15 Nitambariki kwa kumpa mahitaji tele: nitashibisha maskini wake kwa chakula.
I will abundantly bless her provision: I will satisfy her poor with bread.
16 Nitawavika makuhani wake wokovu, nao watakatifu wake watadumu wakiimba kwa furaha.
I will also clothe her priests with salvation: and her saints shall shout aloud for joy.
17 “Hapa nitamchipushia Daudi pembe, na kuweka taa kwa ajili ya masiya wangu.
There will I make the horn of David to bud: I have ordained a lamp for my anointed.
18 Adui zake nitawavika aibu, bali taji kichwani pake itangʼaa sana.”
His enemies will I clothe with shame: but on himself shall his crown flourish.

< Zaburi 132 >