< Zaburi 132 >

1 Wimbo wa kwenda juu. Ee Bwana, mkumbuke Daudi na taabu zote alizozistahimili.
A song of degrees. Lord, remember Dauid with all his affliction.
2 Aliapa kiapo kwa Bwana na akaweka nadhiri kwa Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo:
Who sware vnto the Lord, and vowed vnto the mightie God of Iaakob, saying,
3 “Sitaingia nyumbani mwangu au kwenda kitandani mwangu:
I will not enter into the tabernacle of mine house, nor come vpon my pallet or bed,
4 sitaruhusu usingizi katika macho yangu, wala kope zangu kusinzia,
Nor suffer mine eyes to sleepe, nor mine eye lids to slumber,
5 mpaka nitakapompatia Bwana mahali, makao kwa ajili ya Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo.”
Vntill I finde out a place for the Lord, an habitation for the mightie God of Iaakob.
6 Tulisikia habari hii huko Efrathi, tulikutana nayo katika mashamba ya Yaara:
Lo, we heard of it in Ephrathah, and found it in the fieldes of the forest.
7 “Twendeni kwenye makao yake, na tuabudu kwenye kiti cha kuwekea miguu yake;
We will enter into his Tabernacles, and worship before his footestoole.
8 inuka, Ee Bwana, uje mahali pako pa kupumzikia, wewe na Sanduku la nguvu zako.
Arise, O Lord, to come into thy rest, thou, and the Arke of thy strength.
9 Makuhani wako na wavikwe haki, watakatifu wako na waimbe kwa furaha.”
Let thy Priests be clothed with righteousnesse, and let thy Saints reioyce.
10 Kwa ajili ya Daudi mtumishi wako, usimkatae mpakwa mafuta wako.
For thy seruant Dauids sake refuse not the face of thine Anointed.
11 Bwana alimwapia Daudi kiapo, kiapo cha uhakika ambacho hatakitangua: “Nitamweka mmoja wa wazao wako mwenyewe katika kiti chako cha enzi,
The Lord hath sworne in trueth vnto Dauid, and he wil not shrinke from it, saying, Of the fruite of thy body will I set vpon thy throne.
12 kama wanao watashika Agano langu na sheria ninazowafundisha, ndipo wana wao watarithi kiti chako cha enzi milele na milele.”
If thy sonnes keepe my couenant, and my testimonies, that I shall teach them, their sonnes also shall sit vpon thy throne for euer.
13 Kwa maana Bwana ameichagua Sayuni, amepaonea shauku pawe maskani yake:
For the Lord hath chosen Zion, and loued to dwell in it, saying,
14 “Hapa ni mahali pangu pa kupumzika milele na milele; hapa ndipo nitakapoketi nikitawala, kwa sababu nimepaonea shauku:
This is my rest for euer: here will I dwell, for I haue a delite therein.
15 Nitambariki kwa kumpa mahitaji tele: nitashibisha maskini wake kwa chakula.
I will surely blesse her vitailes, and will satisfie her poore with bread,
16 Nitawavika makuhani wake wokovu, nao watakatifu wake watadumu wakiimba kwa furaha.
And will clothe her Priests with saluation, and her Saints shall shoute for ioye.
17 “Hapa nitamchipushia Daudi pembe, na kuweka taa kwa ajili ya masiya wangu.
There will I make the horne of Dauid to bud: for I haue ordeined a light for mine Anoynted.
18 Adui zake nitawavika aibu, bali taji kichwani pake itangʼaa sana.”
His enemies will I clothe with shame, but on him his crowne shall florish.

< Zaburi 132 >