< Zaburi 132 >
1 Wimbo wa kwenda juu. Ee Bwana, mkumbuke Daudi na taabu zote alizozistahimili.
Een bedevaartslied. Blijf David gedenken, o Jahweh, En alle moeite, die hij zich troostte,
2 Aliapa kiapo kwa Bwana na akaweka nadhiri kwa Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo:
Omdat hij Jahweh had gezworen, Jakobs Sterke had beloofd:
3 “Sitaingia nyumbani mwangu au kwenda kitandani mwangu:
Ik zal mijn woontent niet ingaan, Mijn legerstede niet beklimmen,
4 sitaruhusu usingizi katika macho yangu, wala kope zangu kusinzia,
Mijn ogen geen slaap gunnen, Mijn wimpers geen sluimer:
5 mpaka nitakapompatia Bwana mahali, makao kwa ajili ya Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo.”
Voordat ik een plaats heb gevonden voor Jahweh, Voor Jakobs Sterke een woning!
6 Tulisikia habari hii huko Efrathi, tulikutana nayo katika mashamba ya Yaara:
Zie, wij hoorden, dat zij in Efráta was, Wij vonden haar weer in de velden van Jáar;
7 “Twendeni kwenye makao yake, na tuabudu kwenye kiti cha kuwekea miguu yake;
Laat ons naar zijn Woning gaan, En ons voor zijn voetbank werpen!
8 inuka, Ee Bwana, uje mahali pako pa kupumzikia, wewe na Sanduku la nguvu zako.
Jahweh, trek op naar uw rustplaats, Gij zelf en de ark uwer glorie!
9 Makuhani wako na wavikwe haki, watakatifu wako na waimbe kwa furaha.”
Mogen uw priesters met gerechtigheid worden bekleed, En uw vromen een jubellied zingen!
10 Kwa ajili ya Daudi mtumishi wako, usimkatae mpakwa mafuta wako.
Om wille van David, uw dienaar, Wijs het gebed van uw gezalfde niet af!
11 Bwana alimwapia Daudi kiapo, kiapo cha uhakika ambacho hatakitangua: “Nitamweka mmoja wa wazao wako mwenyewe katika kiti chako cha enzi,
En Jahweh heeft aan David gezworen, Een trouwe Belofte, waarvan Hij niet afwijkt: Van de vrucht van uw schoot Zet Ik er een op uw troon!
12 kama wanao watashika Agano langu na sheria ninazowafundisha, ndipo wana wao watarithi kiti chako cha enzi milele na milele.”
En zo uw zonen mijn verbond onderhouden, En de vermaningen, die Ik hun gaf, Dan zullen ook hùn zonen voor eeuwig Op uw troon blijven zitten!
13 Kwa maana Bwana ameichagua Sayuni, amepaonea shauku pawe maskani yake:
Want Jahweh heeft Sion verkoren, En Zich tot woning begeerd!
14 “Hapa ni mahali pangu pa kupumzika milele na milele; hapa ndipo nitakapoketi nikitawala, kwa sababu nimepaonea shauku:
"Hij is mijn rustplaats voor eeuwig; Hier wil Ik wonen, want hèm heb Ik verkoren!
15 Nitambariki kwa kumpa mahitaji tele: nitashibisha maskini wake kwa chakula.
Zijn mondkost zal Ik ruimschoots zegenen, Zijn armen verzadigen met brood;
16 Nitawavika makuhani wake wokovu, nao watakatifu wake watadumu wakiimba kwa furaha.
Zijn priesters zal Ik met heil bekleden. Zijn vromen zullen een jubellied zingen!
17 “Hapa nitamchipushia Daudi pembe, na kuweka taa kwa ajili ya masiya wangu.
Hier zal Ik David een Hoorn doen ontspruiten, Een lamp ontsteken voor mijn Gezalfde;
18 Adui zake nitawavika aibu, bali taji kichwani pake itangʼaa sana.”
Zijn vijanden zal Ik met schande bedekken, Mijn kroon zal schitteren op zijn hoofd!"