< Zaburi 132 >

1 Wimbo wa kwenda juu. Ee Bwana, mkumbuke Daudi na taabu zote alizozistahimili.
上行之诗。 耶和华啊,求你记念大卫所受的一切苦难!
2 Aliapa kiapo kwa Bwana na akaweka nadhiri kwa Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo:
他怎样向耶和华起誓, 向雅各的大能者许愿,
3 “Sitaingia nyumbani mwangu au kwenda kitandani mwangu:
说:我必不进我的帐幕, 也不上我的床榻;
4 sitaruhusu usingizi katika macho yangu, wala kope zangu kusinzia,
我不容我的眼睛睡觉, 也不容我的眼目打盹;
5 mpaka nitakapompatia Bwana mahali, makao kwa ajili ya Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo.”
直等我为耶和华寻得所在, 为雅各的大能者寻得居所。
6 Tulisikia habari hii huko Efrathi, tulikutana nayo katika mashamba ya Yaara:
我们听说约柜在以法他, 我们在基列·耶琳就寻见了。
7 “Twendeni kwenye makao yake, na tuabudu kwenye kiti cha kuwekea miguu yake;
我们要进他的居所, 在他脚凳前下拜。
8 inuka, Ee Bwana, uje mahali pako pa kupumzikia, wewe na Sanduku la nguvu zako.
耶和华啊,求你兴起, 和你有能力的约柜同入安息之所!
9 Makuhani wako na wavikwe haki, watakatifu wako na waimbe kwa furaha.”
愿你的祭司披上公义! 愿你的圣民欢呼!
10 Kwa ajili ya Daudi mtumishi wako, usimkatae mpakwa mafuta wako.
求你因你仆人大卫的缘故, 不要厌弃你的受膏者!
11 Bwana alimwapia Daudi kiapo, kiapo cha uhakika ambacho hatakitangua: “Nitamweka mmoja wa wazao wako mwenyewe katika kiti chako cha enzi,
耶和华向大卫、凭诚实起了誓, 必不反复,说: 我要使你所生的 坐在你的宝座上。
12 kama wanao watashika Agano langu na sheria ninazowafundisha, ndipo wana wao watarithi kiti chako cha enzi milele na milele.”
你的众子若守我的约 和我所教训他们的法度, 他们的子孙必永远坐在你的宝座上。
13 Kwa maana Bwana ameichagua Sayuni, amepaonea shauku pawe maskani yake:
因为耶和华拣选了锡安, 愿意当作自己的居所,
14 “Hapa ni mahali pangu pa kupumzika milele na milele; hapa ndipo nitakapoketi nikitawala, kwa sababu nimepaonea shauku:
说:这是我永远安息之所; 我要住在这里, 因为是我所愿意的。
15 Nitambariki kwa kumpa mahitaji tele: nitashibisha maskini wake kwa chakula.
我要使其中的粮食丰满, 使其中的穷人饱足。
16 Nitawavika makuhani wake wokovu, nao watakatifu wake watadumu wakiimba kwa furaha.
我要使祭司披上救恩, 圣民大声欢呼!
17 “Hapa nitamchipushia Daudi pembe, na kuweka taa kwa ajili ya masiya wangu.
我要叫大卫的角在那里发生; 我为我的受膏者预备明灯。
18 Adui zake nitawavika aibu, bali taji kichwani pake itangʼaa sana.”
我要使他的仇敌披上羞耻; 但他的冠冕要在头上发光。

< Zaburi 132 >