< Zaburi 130 >
1 Wimbo wa kwenda juu. Kutoka vilindini ninakulilia, Ee Bwana.
Hac ilahisi Derinliklerden sana sesleniyorum, ya RAB,
2 Ee Bwana, sikia sauti yangu. Masikio yako na yawe masikivu kwa kilio changu unihurumie.
Sesimi işit, ya Rab, Yalvarışıma iyi kulak ver!
3 Kama wewe, Ee Bwana, ungeweka kumbukumbu ya dhambi, Ee Bwana, ni nani angeliweza kusimama?
Ya RAB, sen suçların hesabını tutsan, Kim ayakta kalabilir, ya Rab?
4 Lakini kwako kuna msamaha, kwa hiyo wewe unaogopwa.
Ama sen bağışlayıcısın, Öyle ki senden korkulsun.
5 Namngojea Bwana, nafsi yangu inangojea, katika neno lake naweka tumaini langu.
RAB'bi gözlüyorum, Canım RAB'bi gözlüyor, Umut bağlıyorum O'nun sözüne.
6 Nafsi yangu inamngojea Bwana kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi, naam, kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi.
Sabahı gözleyenlerden, Evet, sabahı gözleyenlerden daha çok, Canım Rab'bi gözlüyor.
7 Ee Israeli, mtumaini Bwana, maana kwa Bwana kuna upendo usiokoma, na kwake kuna ukombozi kamili.
Ey İsrail, RAB'be umut bağla! Çünkü RAB'de sevgi, Tam kurtuluş vardır.
8 Yeye mwenyewe ataikomboa Israeli kutoka dhambi zao zote.
İsrail'i bütün suçlarından Fidyeyle O kurtaracaktır.