< Zaburi 130 >

1 Wimbo wa kwenda juu. Kutoka vilindini ninakulilia, Ee Bwana.
De los profundos te llamo, o! Jehová.
2 Ee Bwana, sikia sauti yangu. Masikio yako na yawe masikivu kwa kilio changu unihurumie.
Señor, oye mi voz. Sean tus orejas atentas a la voz de mi oración.
3 Kama wewe, Ee Bwana, ungeweka kumbukumbu ya dhambi, Ee Bwana, ni nani angeliweza kusimama?
Jehová, si mirares a los pecados, Señor ¿quién persistirá?
4 Lakini kwako kuna msamaha, kwa hiyo wewe unaogopwa.
Por lo cual hay perdón acerca de ti: para que seas temido.
5 Namngojea Bwana, nafsi yangu inangojea, katika neno lake naweka tumaini langu.
Yo esperé a Jehová, mi alma esperó: a su palabra he esperado.
6 Nafsi yangu inamngojea Bwana kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi, naam, kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi.
Mi alma esperó a Jehová, más que las guardas esperan a la mañana: las guardas a la mañana.
7 Ee Israeli, mtumaini Bwana, maana kwa Bwana kuna upendo usiokoma, na kwake kuna ukombozi kamili.
Espere Israel a Jehová, porque con Jehová está la misericordia; y abundante redención cerca de él.
8 Yeye mwenyewe ataikomboa Israeli kutoka dhambi zao zote.
Y él redimirá a Israel de todos sus pecados.

< Zaburi 130 >