< Zaburi 130 >

1 Wimbo wa kwenda juu. Kutoka vilindini ninakulilia, Ee Bwana.
Pesem preizvrstna. Iz globočin sem te klical, Gospod:
2 Ee Bwana, sikia sauti yangu. Masikio yako na yawe masikivu kwa kilio changu unihurumie.
Gospod, poslušaj glas moj; ušesa tvoja naj pazijo na prošinj mojih glas.
3 Kama wewe, Ee Bwana, ungeweka kumbukumbu ya dhambi, Ee Bwana, ni nani angeliweza kusimama?
Ako bodeš na krivice gledal, Gospod, kdo bi mogel obstati?
4 Lakini kwako kuna msamaha, kwa hiyo wewe unaogopwa.
Ker pri tebi je odpuščenje, da te česté v svetem strahu.
5 Namngojea Bwana, nafsi yangu inangojea, katika neno lake naweka tumaini langu.
Čakal sem Gospoda, čakala je duša moja; tudi v besedi njegovi imam nado.
6 Nafsi yangu inamngojea Bwana kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi, naam, kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi.
Srce moje hrepeni po Gospodu, bolj ko straže po jutru, ki čujejo noter do jutra.
7 Ee Israeli, mtumaini Bwana, maana kwa Bwana kuna upendo usiokoma, na kwake kuna ukombozi kamili.
Nado imej Izrael v Gospodu, ker pri Gospodu je milost, in pri njem največ rešenja.
8 Yeye mwenyewe ataikomboa Israeli kutoka dhambi zao zote.
In on bode rešil Izrael vseh krivic njegovih.

< Zaburi 130 >