< Zaburi 130 >

1 Wimbo wa kwenda juu. Kutoka vilindini ninakulilia, Ee Bwana.
שיר המעלות ממעמקים קראתיך יהוה׃
2 Ee Bwana, sikia sauti yangu. Masikio yako na yawe masikivu kwa kilio changu unihurumie.
אדני שמעה בקולי תהיינה אזניך קשבות לקול תחנוני׃
3 Kama wewe, Ee Bwana, ungeweka kumbukumbu ya dhambi, Ee Bwana, ni nani angeliweza kusimama?
אם עונות תשמר יה אדני מי יעמד׃
4 Lakini kwako kuna msamaha, kwa hiyo wewe unaogopwa.
כי עמך הסליחה למען תורא׃
5 Namngojea Bwana, nafsi yangu inangojea, katika neno lake naweka tumaini langu.
קויתי יהוה קותה נפשי ולדברו הוחלתי׃
6 Nafsi yangu inamngojea Bwana kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi, naam, kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi.
נפשי לאדני משמרים לבקר שמרים לבקר׃
7 Ee Israeli, mtumaini Bwana, maana kwa Bwana kuna upendo usiokoma, na kwake kuna ukombozi kamili.
יחל ישראל אל יהוה כי עם יהוה החסד והרבה עמו פדות׃
8 Yeye mwenyewe ataikomboa Israeli kutoka dhambi zao zote.
והוא יפדה את ישראל מכל עונתיו׃

< Zaburi 130 >