< Zaburi 130 >
1 Wimbo wa kwenda juu. Kutoka vilindini ninakulilia, Ee Bwana.
Wallfahrtslieder. Aus der Tiefe rufe ich dich, Jahwe,
2 Ee Bwana, sikia sauti yangu. Masikio yako na yawe masikivu kwa kilio changu unihurumie.
Herr, höre auf meine Stimme! Möchten deine Ohren aufmerksam sein auf mein lautes Flehn!
3 Kama wewe, Ee Bwana, ungeweka kumbukumbu ya dhambi, Ee Bwana, ni nani angeliweza kusimama?
Wenn du Verschuldungen im Gedächtnis bewahrtest, Jah, Herr, wer kann dann bestehen?
4 Lakini kwako kuna msamaha, kwa hiyo wewe unaogopwa.
Vielmehr, bei dir steht die Vergebung, damit man dich fürchte.
5 Namngojea Bwana, nafsi yangu inangojea, katika neno lake naweka tumaini langu.
Ich harre auf Jahwe; meine Seele harrt auf sein Wort.
6 Nafsi yangu inamngojea Bwana kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi, naam, kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi.
Innig warte ich auf den Herrn, sehnsüchtiger, als Wächter auf den Morgen, als Wächter auf den Morgen.
7 Ee Israeli, mtumaini Bwana, maana kwa Bwana kuna upendo usiokoma, na kwake kuna ukombozi kamili.
Harre, Israel, auf Jahwe! Denn bei Jahwe ist die Gnade und bei ihm Erlösung in Fülle,
8 Yeye mwenyewe ataikomboa Israeli kutoka dhambi zao zote.
und er wird Israel erlösen von allen seinen Verschuldungen.