< Zaburi 130 >

1 Wimbo wa kwenda juu. Kutoka vilindini ninakulilia, Ee Bwana.
Cantique de Maaloth. O Éternel, je t'invoque des lieux profonds.
2 Ee Bwana, sikia sauti yangu. Masikio yako na yawe masikivu kwa kilio changu unihurumie.
Seigneur, écoute ma voix! Que tes oreilles soient attentives à la voix de mes supplications!
3 Kama wewe, Ee Bwana, ungeweka kumbukumbu ya dhambi, Ee Bwana, ni nani angeliweza kusimama?
Éternel, si tu prends garde aux iniquités, Seigneur, qui subsistera?
4 Lakini kwako kuna msamaha, kwa hiyo wewe unaogopwa.
Mais le pardon se trouve auprès de toi, afin qu'on te craigne.
5 Namngojea Bwana, nafsi yangu inangojea, katika neno lake naweka tumaini langu.
J'ai attendu l'Éternel; mon âme l'a attendu, et j'ai eu mon espérance en sa parole.
6 Nafsi yangu inamngojea Bwana kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi, naam, kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi.
Mon âme attend le Seigneur, plus que les sentinelles n'attendent le matin.
7 Ee Israeli, mtumaini Bwana, maana kwa Bwana kuna upendo usiokoma, na kwake kuna ukombozi kamili.
Israël, attends-toi à l'Éternel, car la miséricorde est auprès de l'Éternel, et la rédemption se trouve en abondance auprès de lui.
8 Yeye mwenyewe ataikomboa Israeli kutoka dhambi zao zote.
Et lui-même rachètera Israël de toutes ses iniquités.

< Zaburi 130 >