< Zaburi 130 >
1 Wimbo wa kwenda juu. Kutoka vilindini ninakulilia, Ee Bwana.
Cantique Mahaloth. Ô Éternel! je t'invoque des lieux profonds.
2 Ee Bwana, sikia sauti yangu. Masikio yako na yawe masikivu kwa kilio changu unihurumie.
Seigneur, écoute ma voix! que tes oreilles soient attentives à la voix de mes supplications.
3 Kama wewe, Ee Bwana, ungeweka kumbukumbu ya dhambi, Ee Bwana, ni nani angeliweza kusimama?
Ô Eternel! si tu prends garde aux iniquités, Seigneur, qui est-ce qui subsistera?
4 Lakini kwako kuna msamaha, kwa hiyo wewe unaogopwa.
Mais il y a pardon par-devers toi, afin que tu sois craint.
5 Namngojea Bwana, nafsi yangu inangojea, katika neno lake naweka tumaini langu.
J'ai attendu l'Eternel; mon âme l'a attendu, et j'ai eu mon attente en sa parole.
6 Nafsi yangu inamngojea Bwana kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi, naam, kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi.
Mon âme [attend] le Seigneur plus que les sentinelles [n'attendent] le matin, plus que les sentinelles [n'attendent] le matin.
7 Ee Israeli, mtumaini Bwana, maana kwa Bwana kuna upendo usiokoma, na kwake kuna ukombozi kamili.
Israël, attends-toi à l'Eternel: car l'Eternel est miséricordieux et il y a rédemption en abondance par devers lui.
8 Yeye mwenyewe ataikomboa Israeli kutoka dhambi zao zote.
Et lui-même rachètera Israël de toutes ses iniquités.