< Zaburi 130 >
1 Wimbo wa kwenda juu. Kutoka vilindini ninakulilia, Ee Bwana.
Kanto de suprenirado. El profundo mi vokas Vin, ho Eternulo.
2 Ee Bwana, sikia sauti yangu. Masikio yako na yawe masikivu kwa kilio changu unihurumie.
Mia Sinjoro, aŭskultu mian voĉon; Viaj oreloj atentu la voĉon de mia petego.
3 Kama wewe, Ee Bwana, ungeweka kumbukumbu ya dhambi, Ee Bwana, ni nani angeliweza kusimama?
Se vi, ho Eternulo, kalkulus la pekojn, Kiu povus stari, ho mia Sinjoro?
4 Lakini kwako kuna msamaha, kwa hiyo wewe unaogopwa.
Sed Vi estas pardonema, Por ke Vi estu respektata.
5 Namngojea Bwana, nafsi yangu inangojea, katika neno lake naweka tumaini langu.
Mi esperis al la Eternulo, esperis mia animo, Kaj Lian vorton mi fidis.
6 Nafsi yangu inamngojea Bwana kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi, naam, kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi.
Mia animo atendas mian Sinjoron pli, Ol la gardantoj atendas la matenon, La gardantoj la matenon.
7 Ee Israeli, mtumaini Bwana, maana kwa Bwana kuna upendo usiokoma, na kwake kuna ukombozi kamili.
Izrael fidu la Eternulon; Ĉar ĉe la Eternulo estas favorkoreco Kaj ĉe Li estas granda liberigo.
8 Yeye mwenyewe ataikomboa Israeli kutoka dhambi zao zote.
Kaj Li liberigos Izraelon De ĉiuj liaj pekoj.