< Zaburi 130 >

1 Wimbo wa kwenda juu. Kutoka vilindini ninakulilia, Ee Bwana.
A Song of the Ascents. From depths I have called Thee, Jehovah.
2 Ee Bwana, sikia sauti yangu. Masikio yako na yawe masikivu kwa kilio changu unihurumie.
Lord, hearken to my voice, Thine ears are attentive to the voice of my supplications.
3 Kama wewe, Ee Bwana, ungeweka kumbukumbu ya dhambi, Ee Bwana, ni nani angeliweza kusimama?
If iniquities Thou dost observe, O Lord, who doth stand?
4 Lakini kwako kuna msamaha, kwa hiyo wewe unaogopwa.
But with Thee [is] forgiveness, that Thou mayest be feared.
5 Namngojea Bwana, nafsi yangu inangojea, katika neno lake naweka tumaini langu.
I hoped [for] Jehovah — hoped hath my soul, And for His word I have waited.
6 Nafsi yangu inamngojea Bwana kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi, naam, kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi.
My soul [is] for the Lord, More than those watching for morning, Watching for morning!
7 Ee Israeli, mtumaini Bwana, maana kwa Bwana kuna upendo usiokoma, na kwake kuna ukombozi kamili.
Israel doth wait on Jehovah, For with Jehovah [is] kindness, And abundant with Him [is] redemption.
8 Yeye mwenyewe ataikomboa Israeli kutoka dhambi zao zote.
And He doth redeem Israel from all his iniquities!

< Zaburi 130 >