< Zaburi 130 >
1 Wimbo wa kwenda juu. Kutoka vilindini ninakulilia, Ee Bwana.
[the] song of The ascents from [the] depths I call out to you O Yahweh.
2 Ee Bwana, sikia sauti yangu. Masikio yako na yawe masikivu kwa kilio changu unihurumie.
O Lord listen! to voice my may they be ears your attentive to [the] sound of supplications my.
3 Kama wewe, Ee Bwana, ungeweka kumbukumbu ya dhambi, Ee Bwana, ni nani angeliweza kusimama?
If iniquities you will keep O Yahweh O Lord who? will he stand.
4 Lakini kwako kuna msamaha, kwa hiyo wewe unaogopwa.
For [is] with you forgiveness so that you may be feared.
5 Namngojea Bwana, nafsi yangu inangojea, katika neno lake naweka tumaini langu.
I wait for Yahweh it waits self my and for word his I hope.
6 Nafsi yangu inamngojea Bwana kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi, naam, kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi.
Self my for [the] Lord more than watchmen for the morning watchmen for the morning.
7 Ee Israeli, mtumaini Bwana, maana kwa Bwana kuna upendo usiokoma, na kwake kuna ukombozi kamili.
Hope O Israel to Yahweh for [is] with Yahweh covenant loyalty and great [is] with him redemption.
8 Yeye mwenyewe ataikomboa Israeli kutoka dhambi zao zote.
And he he will redeem Israel from all iniquities its.