< Zaburi 130 >

1 Wimbo wa kwenda juu. Kutoka vilindini ninakulilia, Ee Bwana.
“A song of the degrees.” Out of the depths have I called thee, O Lord.
2 Ee Bwana, sikia sauti yangu. Masikio yako na yawe masikivu kwa kilio changu unihurumie.
Lord, listen to my voice: let thy ears be attentive to the voice of my supplications.
3 Kama wewe, Ee Bwana, ungeweka kumbukumbu ya dhambi, Ee Bwana, ni nani angeliweza kusimama?
If thou, Lord, shouldst treasure up iniquities, O Lord, who would be able to stand?
4 Lakini kwako kuna msamaha, kwa hiyo wewe unaogopwa.
But with thee there is forgiveness, in order that thou mayest be feared.
5 Namngojea Bwana, nafsi yangu inangojea, katika neno lake naweka tumaini langu.
I hope for the Lord, my soul doth hope, and for his word do I wait.
6 Nafsi yangu inamngojea Bwana kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi, naam, kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi.
My soul [waiteth] for the Lord, more than they that watch for the morning expect the morning.
7 Ee Israeli, mtumaini Bwana, maana kwa Bwana kuna upendo usiokoma, na kwake kuna ukombozi kamili.
Let Israel wait for the Lord; for with the Lord there is kindness, and with him is redemption in abundance;
8 Yeye mwenyewe ataikomboa Israeli kutoka dhambi zao zote.
And he wilt surely redeem Israel from all his iniquities.

< Zaburi 130 >