< Zaburi 130 >

1 Wimbo wa kwenda juu. Kutoka vilindini ninakulilia, Ee Bwana.
Out of the depths I have cried to thee, O Lord:
2 Ee Bwana, sikia sauti yangu. Masikio yako na yawe masikivu kwa kilio changu unihurumie.
Lord, hear my voice. Let thy ears be attentive to the voice of my supplication.
3 Kama wewe, Ee Bwana, ungeweka kumbukumbu ya dhambi, Ee Bwana, ni nani angeliweza kusimama?
If thou, O Lord, wilt mark iniquities: Lord, who shall stand it.
4 Lakini kwako kuna msamaha, kwa hiyo wewe unaogopwa.
For with thee there is merciful forgiveness: and by reason of thy law, I have waited for thee, O Lord. My soul hath relied on his word:
5 Namngojea Bwana, nafsi yangu inangojea, katika neno lake naweka tumaini langu.
My soul hath hoped in the Lord.
6 Nafsi yangu inamngojea Bwana kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi, naam, kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi.
From the morning watch even until night, let Israel hope in the Lord.
7 Ee Israeli, mtumaini Bwana, maana kwa Bwana kuna upendo usiokoma, na kwake kuna ukombozi kamili.
Because with the Lord there is mercy: and with him plentiful redemption.
8 Yeye mwenyewe ataikomboa Israeli kutoka dhambi zao zote.
And he shall redeem Israel from all his iniquities.

< Zaburi 130 >