< Zaburi 130 >

1 Wimbo wa kwenda juu. Kutoka vilindini ninakulilia, Ee Bwana.
A song of ascents. Out of the depths I cry to You, O LORD!
2 Ee Bwana, sikia sauti yangu. Masikio yako na yawe masikivu kwa kilio changu unihurumie.
O Lord, hear my voice; let Your ears be attentive to my plea for mercy.
3 Kama wewe, Ee Bwana, ungeweka kumbukumbu ya dhambi, Ee Bwana, ni nani angeliweza kusimama?
If You, O LORD, kept track of iniquities, then who, O Lord, could stand?
4 Lakini kwako kuna msamaha, kwa hiyo wewe unaogopwa.
But with You there is forgiveness, so that You may be feared.
5 Namngojea Bwana, nafsi yangu inangojea, katika neno lake naweka tumaini langu.
I wait for the LORD; my soul does wait, and in His word I put my hope.
6 Nafsi yangu inamngojea Bwana kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi, naam, kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi.
My soul waits for the Lord more than watchmen wait for the morning— more than watchmen wait for the morning.
7 Ee Israeli, mtumaini Bwana, maana kwa Bwana kuna upendo usiokoma, na kwake kuna ukombozi kamili.
O Israel, put your hope in the LORD, for with the LORD is loving devotion, and with Him is redemption in abundance.
8 Yeye mwenyewe ataikomboa Israeli kutoka dhambi zao zote.
And He will redeem Israel from all iniquity.

< Zaburi 130 >