< Zaburi 130 >
1 Wimbo wa kwenda juu. Kutoka vilindini ninakulilia, Ee Bwana.
Een lied Hammaaloth. Uit de diepten roep ik tot U, o HEERE!
2 Ee Bwana, sikia sauti yangu. Masikio yako na yawe masikivu kwa kilio changu unihurumie.
HEERE! hoor naar mijn stem; laat Uw oren opmerkende zijn op de stem mijner smekingen.
3 Kama wewe, Ee Bwana, ungeweka kumbukumbu ya dhambi, Ee Bwana, ni nani angeliweza kusimama?
Zo Gij, HEERE! de ongerechtigheden gadeslaat; HEERE! wie zal bestaan?
4 Lakini kwako kuna msamaha, kwa hiyo wewe unaogopwa.
Maar bij U is vergeving, opdat Gij gevreesd wordt.
5 Namngojea Bwana, nafsi yangu inangojea, katika neno lake naweka tumaini langu.
Ik verwacht den HEERE; mijn ziel verwacht, en ik hoop op Zijn Woord.
6 Nafsi yangu inamngojea Bwana kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi, naam, kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi.
Mijn ziel wacht op den HEERE, meer dan de wachters op den morgen; de wachters op den morgen.
7 Ee Israeli, mtumaini Bwana, maana kwa Bwana kuna upendo usiokoma, na kwake kuna ukombozi kamili.
Israel hope op den HEERE; want bij den HEERE is goedertierenheid, en bij Hem is veel verlossing.
8 Yeye mwenyewe ataikomboa Israeli kutoka dhambi zao zote.
En Hij zal Israel verlossen van al zijn ongerechtigheden.