< Zaburi 130 >

1 Wimbo wa kwenda juu. Kutoka vilindini ninakulilia, Ee Bwana.
上行之詩。 耶和華啊,我從深處向你求告!
2 Ee Bwana, sikia sauti yangu. Masikio yako na yawe masikivu kwa kilio changu unihurumie.
主啊,求你聽我的聲音! 願你側耳聽我懇求的聲音!
3 Kama wewe, Ee Bwana, ungeweka kumbukumbu ya dhambi, Ee Bwana, ni nani angeliweza kusimama?
主-耶和華啊,你若究察罪孽, 誰能站得住呢?
4 Lakini kwako kuna msamaha, kwa hiyo wewe unaogopwa.
但在你有赦免之恩, 要叫人敬畏你。
5 Namngojea Bwana, nafsi yangu inangojea, katika neno lake naweka tumaini langu.
我等候耶和華,我的心等候; 我也仰望他的話。
6 Nafsi yangu inamngojea Bwana kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi, naam, kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi.
我的心等候主, 勝於守夜的,等候天亮, 勝於守夜的,等候天亮。
7 Ee Israeli, mtumaini Bwana, maana kwa Bwana kuna upendo usiokoma, na kwake kuna ukombozi kamili.
以色列啊,你當仰望耶和華! 因他有慈愛,有豐盛的救恩。
8 Yeye mwenyewe ataikomboa Israeli kutoka dhambi zao zote.
他必救贖以色列脫離一切的罪孽。

< Zaburi 130 >