< Zaburi 130 >
1 Wimbo wa kwenda juu. Kutoka vilindini ninakulilia, Ee Bwana.
Y Cantan Quinajulo. Y sumanjiyong y tinadong nae juagang jao, O Jeova.
2 Ee Bwana, sikia sauti yangu. Masikio yako na yawe masikivu kwa kilio changu unihurumie.
Jeova, ecungog y inagangjo: polo ya talangamo sija uegueng gui inagang y guinagaojo.
3 Kama wewe, Ee Bwana, ungeweka kumbukumbu ya dhambi, Ee Bwana, ni nani angeliweza kusimama?
Yanguin mojon unmatca y tinaelaye sija; Jeova, jaye utojgüe?
4 Lakini kwako kuna msamaha, kwa hiyo wewe unaogopwa.
Lao guaja inasie guiya jago, para unmamaañagüe.
5 Namngojea Bwana, nafsi yangu inangojea, katika neno lake naweka tumaini langu.
Junanangga si Jeova, y antijo mannanangga, ya y sinanganña junanangga.
6 Nafsi yangu inamngojea Bwana kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi, naam, kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi.
Y antijo jananangga si Jeova, mas qui y guatdia sija ni manmannanangga y egaan: magajet na mas qui y guatdia sija manmannananangga y egaan.
7 Ee Israeli, mtumaini Bwana, maana kwa Bwana kuna upendo usiokoma, na kwake kuna ukombozi kamili.
O Israel nangga si Jeova; sa gui as Jeova guaja minaase, ya iya guiya nae megae na inalibre.
8 Yeye mwenyewe ataikomboa Israeli kutoka dhambi zao zote.
Ya güiya unalibre Israel todo gui tinaelayeña.