< Zaburi 129 >

1 Wimbo wa kwenda juu. Wamenionea mno tangu ujana wangu; Israeli na aseme sasa:
Muchas veces me persiguieron desde mi juventud. Que [lo] diga ahora Israel:
2 wamenionea mno tangu ujana wangu, lakini bado hawajanishinda.
Muchas veces me persiguieron desde mi juventud, Pero no prevalecieron contra mí.
3 Wakulima wamelima mgongo wangu, na kufanya mifereji yao mirefu.
Los aradores araron sobre mi espalda. Hicieron largos surcos.
4 Lakini Bwana ni mwenye haki; amenifungua toka kamba za waovu.
Yavé es justo, Cortó las cuerdas de los perversos.
5 Wale wote waichukiao Sayuni na warudishwe nyuma kwa aibu.
Sean avergonzados y vueltos atrás Todos los que aborrecen a Sion.
6 Wawe kama majani juu ya paa, ambayo hunyauka kabla hayajakua;
Sean como [la] hierba de las azoteas Que se marchita antes de crecer,
7 kwa hayo mvunaji hawezi kujaza vitanga vyake, wala akusanyaye kujaza mikono yake.
Con la cual el cosechero no llena su mano, Ni el regazo el que ata manojos.
8 Wale wapitao karibu na wasiseme, “Baraka ya Bwana iwe juu yako; tunakubariki katika jina la Bwana.”
Ni le dicen los que pasan: La bendición de Yavé sea sobre ustedes, Los bendecimos en el Nombre de Yavé.

< Zaburi 129 >