< Zaburi 129 >
1 Wimbo wa kwenda juu. Wamenionea mno tangu ujana wangu; Israeli na aseme sasa:
Une chanson d'ascension. Ils m'ont souvent affligé depuis ma jeunesse. Laissez Israël dire maintenant:
2 wamenionea mno tangu ujana wangu, lakini bado hawajanishinda.
maintes fois ils m'ont affligé depuis ma jeunesse, mais ils n'ont pas prévalu contre moi.
3 Wakulima wamelima mgongo wangu, na kufanya mifereji yao mirefu.
Les laboureurs ont labouré sur mon dos. Ils ont tracé de longs sillons.
4 Lakini Bwana ni mwenye haki; amenifungua toka kamba za waovu.
Yahvé est juste. Il a coupé les cordes des méchants.
5 Wale wote waichukiao Sayuni na warudishwe nyuma kwa aibu.
Qu'ils soient déçus et retournent en arrière, tous ceux qui détestent Sion.
6 Wawe kama majani juu ya paa, ambayo hunyauka kabla hayajakua;
Qu'ils soient comme l'herbe sur les toits, qui se fane avant de grandir,
7 kwa hayo mvunaji hawezi kujaza vitanga vyake, wala akusanyaye kujaza mikono yake.
avec lesquels la faucheuse ne remplit pas sa main, ni celui qui lie les gerbes, sa poitrine.
8 Wale wapitao karibu na wasiseme, “Baraka ya Bwana iwe juu yako; tunakubariki katika jina la Bwana.”
Et ceux qui passent ne disent pas non plus, « Que la bénédiction de Yahvé soit sur vous. Nous vous bénissons au nom de Yahvé. »