< Zaburi 129 >

1 Wimbo wa kwenda juu. Wamenionea mno tangu ujana wangu; Israeli na aseme sasa:
“A psalm of the steps, or the goings up.” Much have they afflicted me from my youth, May Israel now say;
2 wamenionea mno tangu ujana wangu, lakini bado hawajanishinda.
Much have they afflicted me from my youth, Yet have they not prevailed against me.
3 Wakulima wamelima mgongo wangu, na kufanya mifereji yao mirefu.
The ploughers ploughed up my back; They made long their furrows;
4 Lakini Bwana ni mwenye haki; amenifungua toka kamba za waovu.
But the LORD was righteous; He cut asunder the cords of the wicked.
5 Wale wote waichukiao Sayuni na warudishwe nyuma kwa aibu.
Let all be driven back with shame Who hate Zion!
6 Wawe kama majani juu ya paa, ambayo hunyauka kabla hayajakua;
Let them be as grass upon the house-tops, Which withereth before one pulleth it up;
7 kwa hayo mvunaji hawezi kujaza vitanga vyake, wala akusanyaye kujaza mikono yake.
With which the reaper filleth not his hand, Nor he that bindeth sheaves his bosom!
8 Wale wapitao karibu na wasiseme, “Baraka ya Bwana iwe juu yako; tunakubariki katika jina la Bwana.”
And they who pass by do not say, “The blessing of the LORD be upon you! We bless you in the name of the LORD!”

< Zaburi 129 >