< Zaburi 129 >
1 Wimbo wa kwenda juu. Wamenionea mno tangu ujana wangu; Israeli na aseme sasa:
“A song of the degrees.” Many a time have they assailed me from my youth, so should Israel say;
2 wamenionea mno tangu ujana wangu, lakini bado hawajanishinda.
Many a time have they assailed me from my youth: yet have they not prevailed against me.
3 Wakulima wamelima mgongo wangu, na kufanya mifereji yao mirefu.
Upon my back have ploughmen ploughed; they have drawn long their furrows:
4 Lakini Bwana ni mwenye haki; amenifungua toka kamba za waovu.
[Yet] the Lord is righteous; he hath cut asunder the cords of the wicked.
5 Wale wote waichukiao Sayuni na warudishwe nyuma kwa aibu.
May all be put to shame and turned backward that hate Zion;
6 Wawe kama majani juu ya paa, ambayo hunyauka kabla hayajakua;
May they become like the grass of the roofs, which withereth before it is pulled up;
7 kwa hayo mvunaji hawezi kujaza vitanga vyake, wala akusanyaye kujaza mikono yake.
Wherewith the mower filleth not his hand; nor his arm he that bindeth sheaves.
8 Wale wapitao karibu na wasiseme, “Baraka ya Bwana iwe juu yako; tunakubariki katika jina la Bwana.”
Nor do they who pass by say, The blessing of the Lord be with you: we bless you in the name of the Lord.