< Zaburi 129 >
1 Wimbo wa kwenda juu. Wamenionea mno tangu ujana wangu; Israeli na aseme sasa:
A song of degrees. They haue often times afflicted me from my youth (may Israel nowe say)
2 wamenionea mno tangu ujana wangu, lakini bado hawajanishinda.
They haue often times afflicted me from my youth: but they could not preuaile against me.
3 Wakulima wamelima mgongo wangu, na kufanya mifereji yao mirefu.
The plowers plowed vpon my backe, and made long furrowes.
4 Lakini Bwana ni mwenye haki; amenifungua toka kamba za waovu.
But the righteous Lord hath cut the cordes of the wicked.
5 Wale wote waichukiao Sayuni na warudishwe nyuma kwa aibu.
They that hate Zion, shalbe all ashamed and turned backward.
6 Wawe kama majani juu ya paa, ambayo hunyauka kabla hayajakua;
They shalbe as the grasse on the house tops, which withereth afore it commeth forth.
7 kwa hayo mvunaji hawezi kujaza vitanga vyake, wala akusanyaye kujaza mikono yake.
Whereof the mower filleth not his hand, neither the glainer his lap:
8 Wale wapitao karibu na wasiseme, “Baraka ya Bwana iwe juu yako; tunakubariki katika jina la Bwana.”
Neither they, which go by, say, The blessing of the Lord be vpon you, or, We blesse you in the Name of the Lord.