< Zaburi 129 >

1 Wimbo wa kwenda juu. Wamenionea mno tangu ujana wangu; Israeli na aseme sasa:
A Canticle in steps. They have often fought against me from my youth, let Israel now say:
2 wamenionea mno tangu ujana wangu, lakini bado hawajanishinda.
they have often fought against me from my youth, yet they could not prevail over me.
3 Wakulima wamelima mgongo wangu, na kufanya mifereji yao mirefu.
The sinners have made fabrications behind my back. They have prolonged their iniquity.
4 Lakini Bwana ni mwenye haki; amenifungua toka kamba za waovu.
The just Lord will cut the necks of sinners.
5 Wale wote waichukiao Sayuni na warudishwe nyuma kwa aibu.
Let all those who hate Zion be confounded and turned backwards.
6 Wawe kama majani juu ya paa, ambayo hunyauka kabla hayajakua;
Let them be like grass on the rooftops, which withers before it can be pulled up:
7 kwa hayo mvunaji hawezi kujaza vitanga vyake, wala akusanyaye kujaza mikono yake.
with it, he who reaps does not fill his hand and he who gathers sheaves does not fill his bosom.
8 Wale wapitao karibu na wasiseme, “Baraka ya Bwana iwe juu yako; tunakubariki katika jina la Bwana.”
And those who were passing by have not said to them: “The blessing of the Lord be upon you. We have blessed you in the name of the Lord.”

< Zaburi 129 >