< Zaburi 129 >

1 Wimbo wa kwenda juu. Wamenionea mno tangu ujana wangu; Israeli na aseme sasa:
A Song of the going up. Great have been my troubles from the time when I was young (let Israel now say);
2 wamenionea mno tangu ujana wangu, lakini bado hawajanishinda.
Great have been my troubles from the time when I was young, but my troubles have not overcome me.
3 Wakulima wamelima mgongo wangu, na kufanya mifereji yao mirefu.
The ploughmen were ploughing on my back; long were the wounds they made.
4 Lakini Bwana ni mwenye haki; amenifungua toka kamba za waovu.
The Lord is true: the cords of the evil-doers are broken in two.
5 Wale wote waichukiao Sayuni na warudishwe nyuma kwa aibu.
Let all the haters of Zion be shamed and turned back.
6 Wawe kama majani juu ya paa, ambayo hunyauka kabla hayajakua;
Let them be like the grass on the house-tops, which is dry before it comes to full growth.
7 kwa hayo mvunaji hawezi kujaza vitanga vyake, wala akusanyaye kujaza mikono yake.
He who gets in the grain has no use for it; and they do not make bands of it for the grain-stems.
8 Wale wapitao karibu na wasiseme, “Baraka ya Bwana iwe juu yako; tunakubariki katika jina la Bwana.”
And those who go by do not say, The blessing of the Lord be on you; we give you blessing in the name of the Lord.

< Zaburi 129 >