< Zaburi 129 >

1 Wimbo wa kwenda juu. Wamenionea mno tangu ujana wangu; Israeli na aseme sasa:
上行之詩。 以色列當說:從我幼年以來, 敵人屢次苦害我,
2 wamenionea mno tangu ujana wangu, lakini bado hawajanishinda.
從我幼年以來,敵人屢次苦害我, 卻沒有勝了我。
3 Wakulima wamelima mgongo wangu, na kufanya mifereji yao mirefu.
如同扶犂的在我背上扶犂而耕, 耕的犂溝甚長。
4 Lakini Bwana ni mwenye haki; amenifungua toka kamba za waovu.
耶和華是公義的; 他砍斷了惡人的繩索。
5 Wale wote waichukiao Sayuni na warudishwe nyuma kwa aibu.
願恨惡錫安的都蒙羞退後!
6 Wawe kama majani juu ya paa, ambayo hunyauka kabla hayajakua;
願他們像房頂上的草, 未長成而枯乾,
7 kwa hayo mvunaji hawezi kujaza vitanga vyake, wala akusanyaye kujaza mikono yake.
收割的不夠一把, 捆禾的也不滿懷。
8 Wale wapitao karibu na wasiseme, “Baraka ya Bwana iwe juu yako; tunakubariki katika jina la Bwana.”
過路的也不說: 願耶和華所賜的福歸與你們! 我們奉耶和華的名給你們祝福!

< Zaburi 129 >