< Zaburi 126 >
1 Wimbo wa kwenda juu. Bwana alipowarejeza mateka Sayuni, tulikuwa kama watu walioota ndoto.
Cuando Yavé devuelva a los cautivos de Sion, Seremos como los que sueñan.
2 Vinywa vyetu vilijaa kicheko, ndimi zetu zilijaa nyimbo za shangwe. Ndipo iliposemwa miongoni mwa mataifa, “Bwana amewatendea mambo makuu.”
Entonces nuestras bocas se llenarán de risa, Y nuestras lenguas de alabanza. Entonces dirán entre las naciones: ¡Grandes cosas hizo Yavé por éstos!
3 Bwana ametutendea mambo makuu, nasi tumejaa furaha.
¡Yavé hizo grandes cosas por nosotros! ¡Estamos alegres!
4 Ee Bwana, turejeshee watu wetu waliotekwa, kama vijito katika Negebu.
Devuelve a nuestros cautivos, oh Yavé, Como los torrentes en el Neguev.
5 Wapandao kwa machozi watavuna kwa nyimbo za shangwe.
Los que siembran con lágrimas Con regocijo segarán.
6 Yeye azichukuaye mbegu zake kwenda kupanda, huku akilia, atarudi kwa nyimbo za shangwe, akichukua miganda ya mavuno yake.
El que va de un lado a otro llorando Y lleva el saco de semilla, Ciertamente volverá con regocijo Y traerá sus manojos.