< Zaburi 125 >
1 Wimbo wa kwenda juu. Wale wamtumainio Bwana ni kama mlima Sayuni, ambao hauwezi kutikisika, bali wadumu milele.
Cantique des degrés. Ceux qui se confient en l’Éternel sont comme la montagne de Sion, qui ne chancelle pas, qui demeure à toujours.
2 Kama milima inavyozunguka Yerusalemu, ndivyo Bwana anavyowazunguka watu wake sasa na hata milele.
Jérusalem! – des montagnes sont autour d’elle, et l’Éternel est autour de son peuple, dès maintenant et à toujours.
3 Fimbo ya waovu haitadumu juu ya nchi waliopewa wenye haki, ili wenye haki wasije wakatumia mikono yao kutenda ubaya.
Car le bâton de la méchanceté ne reposera pas sur le lot des justes; afin que les justes n’étendent pas leur main vers l’iniquité.
4 Ee Bwana, watendee mema walio wema, wale walio wanyofu wa moyo.
Éternel! fais du bien aux gens de bien et à ceux qui sont droits dans leur cœur!
5 Bali wale wanaogeukia njia zilizopotoka, Bwana atawafukuza pamoja na watenda mabaya. Amani iwe juu ya Israeli.
Mais quant à ceux qui se détournent dans leurs voies tortueuses, l’Éternel les fera marcher avec les ouvriers d’iniquité. La paix soit sur Israël!