< Zaburi 125 >

1 Wimbo wa kwenda juu. Wale wamtumainio Bwana ni kama mlima Sayuni, ambao hauwezi kutikisika, bali wadumu milele.
song [the] step [the] to trust in/on/with LORD like/as mountain: mount Zion not to shake to/for forever: enduring to dwell
2 Kama milima inavyozunguka Yerusalemu, ndivyo Bwana anavyowazunguka watu wake sasa na hata milele.
Jerusalem mountain: mount around to/for her and LORD around to/for people his from now and till forever: enduring
3 Fimbo ya waovu haitadumu juu ya nchi waliopewa wenye haki, ili wenye haki wasije wakatumia mikono yao kutenda ubaya.
for not to rest tribe: staff [the] wickedness upon allotted [the] righteous because not to send: reach [the] righteous in/on/with injustice hand their
4 Ee Bwana, watendee mema walio wema, wale walio wanyofu wa moyo.
be good [emph?] LORD to/for pleasant and to/for upright in/on/with heart their
5 Bali wale wanaogeukia njia zilizopotoka, Bwana atawafukuza pamoja na watenda mabaya. Amani iwe juu ya Israeli.
and [the] to stretch crooked their to go: went them LORD with to work [the] evil: wickedness peace upon Israel

< Zaburi 125 >