< Zaburi 125 >
1 Wimbo wa kwenda juu. Wale wamtumainio Bwana ni kama mlima Sayuni, ambao hauwezi kutikisika, bali wadumu milele.
“A psalm of the steps, or the goings up.” They who trust in the LORD shall be as Mount Zion, Which cannot be moved, which standeth for ever.
2 Kama milima inavyozunguka Yerusalemu, ndivyo Bwana anavyowazunguka watu wake sasa na hata milele.
As the mountains are round about Jerusalem, So the LORD is round about his people, Henceforth even for ever!
3 Fimbo ya waovu haitadumu juu ya nchi waliopewa wenye haki, ili wenye haki wasije wakatumia mikono yao kutenda ubaya.
For the sceptre of the wicked shall not remain upon the portion of the righteous, Lest the righteous put forth their hands to iniquity.
4 Ee Bwana, watendee mema walio wema, wale walio wanyofu wa moyo.
Do good, O LORD! to the good, To them that are upright in heart!
5 Bali wale wanaogeukia njia zilizopotoka, Bwana atawafukuza pamoja na watenda mabaya. Amani iwe juu ya Israeli.
But such as turn aside to their crooked ways, -May the LORD destroy them with the evil-doers! Peace be to Israel!