< Zaburi 123 >

1 Wimbo wa kwenda juu. Ninayainua macho yangu kwako, kwako wewe ambaye kiti chako cha enzi kiko mbinguni.
(성전에 올라가는 노래) 하늘에 계신 주여, 내가 눈을 들어 주께 향하나이다
2 Kama vile macho ya watumwa yatazamavyo mkono wa bwana wao, kama vile macho ya mtumishi wa kike yatazamavyo mkono wa bibi yake, ndivyo macho yetu yamtazamavyo Bwana Mungu wetu, mpaka atakapotuhurumia.
종의 눈이 그 상전의 손을 여종의 눈이 그 주모의 손을 바람같이 우리 눈이 여호와 우리 하나님을 바라며 우리를 긍휼히 여기시기를 기다리나이다
3 Uturehemu, Ee Bwana, uturehemu, kwa maana tumevumilia dharau nyingi.
여호와여, 우리를 긍휼히 여기시고 긍휼히 여기소서 심한 멸시가 우리에게 넘치나이다
4 Tumevumilia dhihaka nyingi kutoka kwa wenye kiburi, dharau nyingi kutoka kwa wenye majivuno.
평안한 자의 조소와 교만한 자의 멸시가 우리 심령에 넘치나이다

< Zaburi 123 >