< Zaburi 122 >

1 Wimbo wa kwenda juu. Wa Daudi. Nilishangilia pamoja na wale walioniambia, “Twende nyumbani ya Bwana.”
שיר המעלות לדוד שמחתי באמרים לי-- בית יהוה נלך
2 Ee Yerusalemu, miguu yetu imesimama malangoni mwako.
עמדות היו רגלינו-- בשעריך ירושלם
3 Yerusalemu imejengwa vyema kama mji ambao umeshikamanishwa pamoja.
ירושלם הבנויה-- כעיר שחברה-לה יחדו
4 Huko ndiko makabila hukwea, makabila ya Bwana, kulisifu jina la Bwana kulingana na maagizo waliopewa Israeli.
ששם עלו שבטים שבטי-יה--עדות לישראל להדות לשם יהוה
5 Huko viti vya enzi vya hukumu hukaa, viti vya enzi vya nyumba ya Daudi.
כי שמה ישבו כסאות למשפט כסאות לבית דוד
6 Omba kwa ajili ya amani ya Yerusalemu: “Wote wakupendao na wawe salama.
שאלו שלום ירושלם ישליו אהביך
7 Amani na iwepo ndani ya kuta zako na usalama ndani ya ngome zako.”
יהי-שלום בחילך שלוה בארמנותיך
8 Kwa ajili ya ndugu zangu na marafiki, nitasema, “Amani iwe ndani yako.”
למען אחי ורעי-- אדברה-נא שלום בך
9 Kwa ajili ya nyumba ya Bwana Mungu wetu, nitatafuta mafanikio yako.
למען בית-יהוה אלהינו-- אבקשה טוב לך

< Zaburi 122 >