< Zaburi 122 >

1 Wimbo wa kwenda juu. Wa Daudi. Nilishangilia pamoja na wale walioniambia, “Twende nyumbani ya Bwana.”
Hodočasnička pjesma. Davidova. Obradovah se kad mi rekoše: “Hajdemo u Dom Jahvin!”
2 Ee Yerusalemu, miguu yetu imesimama malangoni mwako.
Eto, noge nam već stoje na vratima tvojim, Jeruzaleme.
3 Yerusalemu imejengwa vyema kama mji ambao umeshikamanishwa pamoja.
Jeruzaleme, grade čvrsto sazdani i kao u jedno saliveni!
4 Huko ndiko makabila hukwea, makabila ya Bwana, kulisifu jina la Bwana kulingana na maagizo waliopewa Israeli.
Onamo uzlaze plemena, plemena Jahvina, po Zakonu Izraelovu, da slave ime Jahvino.
5 Huko viti vya enzi vya hukumu hukaa, viti vya enzi vya nyumba ya Daudi.
Ondje stoje sudačke stolice, stolice doma Davidova.
6 Omba kwa ajili ya amani ya Yerusalemu: “Wote wakupendao na wawe salama.
Molite za mir Jeruzalemov! Blago onima koji tebe ljube!
7 Amani na iwepo ndani ya kuta zako na usalama ndani ya ngome zako.”
Neka bude mir u zidinama tvojim i pokoj u tvojim palačama!
8 Kwa ajili ya ndugu zangu na marafiki, nitasema, “Amani iwe ndani yako.”
Radi braće i prijatelja svojih klicat ću: “Mir tebi!”
9 Kwa ajili ya nyumba ya Bwana Mungu wetu, nitatafuta mafanikio yako.
Radi Doma Jahve, Boga našega, za sreću tvoju ja ću moliti.

< Zaburi 122 >