< Zaburi 12 >
1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa sheminithi. Zaburi ya Daudi. Bwana tusaidie, kwa kuwa wacha Mungu wametoweka; waaminifu wametoweka miongoni mwa wanadamu.
Müzik şefi için - Sekiz telli sazlarla - Davut'un mezmuru Kurtar beni, ya RAB, sadık kulun kalmadı, Güvenilir insanlar yok oldu.
2 Kila mmoja humwambia jirani yake uongo; midomo yao ya hila huzungumza kwa udanganyifu.
Herkes birbirine yalan söylüyor, Dalkavukluk, ikiyüzlülük ediyor.
3 Bwana na akatilie mbali midomo yote ya hila na kila ulimi uliojaa majivuno,
Sustursun RAB dalkavukların ağzını, Büyüklenen dilleri.
4 ule unaosema, “Kwa ndimi zetu tutashinda; midomo ni mali yetu, bwana wetu ni nani?”
Onlar ki, “Dilimizle kazanırız, Dudaklarımız emrimizde, Kim bize efendilik edebilir?” derler.
5 “Kwa sababu ya uonevu wa wanyonge na kulia kwa uchungu kwa wahitaji, nitainuka sasa,” asema Bwana. “Nitawalinda kutokana na wale wenye nia mbaya juu yao.”
“Şimdi kalkacağım” diyor RAB, “Çünkü mazlumlar eziliyor, Yoksullar inliyor, Özledikleri kurtuluşu vereceğim onlara.”
6 Maneno ya Bwana ni safi, kama fedha iliyosafishwa katika tanuru, iliyosafishwa mara saba.
RAB'bin sözleri pak sözlerdir; Toprak ocakta eritilmiş, Yedi kez arıtılmış gümüşe benzer.
7 Ee Bwana, utatuweka salama na kutulinda na kizazi hiki milele.
Sen onları koru, ya RAB, Bu kötü kuşaktan hep uzak tut!
8 Watu waovu huenda wakiringa kila mahali wakati ambapo yule aliye mbaya sana ndiye anayeheshimiwa miongoni mwa watu.
İnsanlar arasında alçaklık rağbet görünce, Kötüler her yanda dolaşır oldu.